-
Kuacha Ibada ya Maliki na Kuanza Ibada ya KweliMnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 1
-
-
Migawo yetu ilibadilika katika 1968 nilipoitwa kwenye ofisi ya tawi katika Tokyo kufanya kazi ya utafsiri. Kwa sababu ya upungufu wa vyumba, nilisafiri kila siku kutoka eneo la Sumida, Tokyo, naye Junko alitumikia akiwa painia wa pekee pamoja na kutaniko la mahali hapo. Kufikia wakati huu, majengo ya ofisi ya tawi makubwa kidogo yalihitajiwa. Hivyo, katika 1970, uwanja ulinunuliwa katika Numazu karibu na Mlima Fuji. Hapo, kiwanda chenye orofa tatu pamoja na nyumba ya makazi zilijengwa. Kabla ya ujenzi kuanza, nyumba kadhaa kwenye uwanja huo zilitumiwa kufanyia Shule ya Huduma ya Ufalme, ambayo huandaa mazoezi kwa waangalizi wa kutaniko.
-
-
Kuacha Ibada ya Maliki na Kuanza Ibada ya KweliMnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 1
-
-
Punde si punde, tuliongezeka tukawa wengi zaidi kuweza kutoshea majengo ya Betheli katika Numazu. Hivyo, ekari 18 za ardhi zilinunuliwa katika Jiji la Ebina, na ujenzi wa ofisi mpya ya tawi ukaanza katika 1978. Sasa nafasi yote iliyopo katika uwanja huu imefunikwa na majengo ya makazi na kiwanda, kutia na Jumba la Mkusanyiko linalotoshea watu zaidi ya 2,800. Nyongeza ya mwisho, inayotia ndani majengo mawili ya makazi yenye orofa 13 na jengo la utumishi na kuegeshea magari lenye sehemu 5, ilimalizika mwanzoni mwa mwaka huu. Familia yetu ya Betheli sasa imefikia washiriki 530, lakini majengo yaliyopanuliwa yataturuhusu kuwapa makao washiriki wapatao 900.
-