Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uvumilivu Huleta Shangwe
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Julai 1
    • Naacha Kuwa Dereva wa Basi na Kuwa Mhubiri

      Mojawapo ya mambo ya kwanza niliyofanya nilipofika Salvador ni kununua Biblia. Baada ya kuhudhuria kanisa la Baptisti kwa miaka kadhaa, nilifanya urafiki na dereva mwenzangu aliyeitwa Durval. Mara nyingi mimi na Durval tulikuwa na mazungumzo mengi ya Biblia. Siku moja alinipa kijitabu chenye kichwa Where Are the Dead?a Ingawa niliamini kwamba wanadamu wana nafsi isiyoweza kufa, nilitaka kuchunguza Maandiko yaliyoonyeshwa katika kijitabu hicho. Nilishangaa kuona uthibitisho wa Biblia kwamba nafsi inayotenda dhambi inakufa.—Ezekieli 18:4.

      Alipoona kwamba ninapendezwa na mazungumzo ya Biblia, Durval alimwomba Antônio Andrade, mtumishi wa wakati wote wa Mashahidi wa Yehova, anitembelee nyumbani. Baada ya kunitembelea mara tatu, Antônio alinialika niambatane naye ili kuwafundisha wengine Biblia. Baada ya kuzungumza kwenye nyumba mbili za kwanza, aliniambia, “Sasa ni zamu yako.” Niliogopa sana lakini nilifurahi kwamba familia moja ilisikiliza kwa makini na wakakubali kupokea vitabu viwili. Mpaka leo mimi hufurahi sana ninapompata mtu anayependezwa na kweli ya Biblia.

      Nilibatizwa katika Bahari ya Atlantiki karibu na Salvador mnamo Aprili 19, 1943, wakati wa maadhimisho ya kifo cha Kristo. Kwa sababu hakukuwa na wanaume Wakristo wenye uzoefu, nilipewa mgawo wa kusaidia kikundi cha Mashahidi waliofanya mikutano katika nyumba ya Ndugu Andrade kwenye mojawapo ya barabara nyembamba zinazounganisha upande wa juu na wa chini wa jiji la Salvador.

      Upinzani Katika Miaka ya Mapema

      Watu hawakupenda utendaji wetu wa Kikristo wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu (1939-1945). Watu fulani wenye mamlaka walifikiri kwamba tulikuwa wapelelezi kutoka Amerika Kaskazini kwa sababu vichapo vyetu vingi vilitoka Marekani. Hivyo, mara nyingi tulikamatwa na kuhojiwa. Shahidi yeyote alipokosa kurudi kutoka katika utumishi wa shambani, tulikata kauli kwamba alifungwa na hivyo tulienda katika kituo cha polisi ili kuomba afunguliwe.

      Mnamo Agosti 1943, Adolphe Messmer, Shahidi Mjerumani, alikuja Salvador kutusaidia kupanga kusanyiko letu la kwanza. Baada ya kupata kibali kutoka kwa wenye mamlaka ili kufanya kusanyiko hilo, hotuba ya watu wote yenye kichwa “Uhuru Katika Ulimwengu Mpya” ilitangazwa magazetini, na matangazo yakabandikwa kwenye madirisha ya maduka na kwenye mabasi. Lakini katika siku ya pili ya kusanyiko, polisi fulani alitufahamisha kwamba kibali chetu cha kukusanyika kilikuwa kimefutwa. Askofu mkuu wa Salvador alimshurutisha mkuu wa polisi asimamishe kusanyiko letu. Hata hivyo, mnamo Aprili mwaka uliofuata, tuliruhusiwa kukusanyika kwa ajili ya ile hotuba ya watu wote iliyokuwa imetangazwa.

  • Uvumilivu Huleta Shangwe
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Julai 1
    • [Picha katika ukurasa wa 9]

      Mashahidi watangaza hotuba ya watu wote katika kusanyiko la kwanza jijini Salvador mwaka wa 1943

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki