Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumtumikia Yehova Tukiwa Familia Iliyoungana
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Oktoba 1
    • Mwenye Furaha Katika Utumishi wa Wakati Wote

      Katika Januari 1954, nilipokuwa mwenye umri wa miaka 22 tu, nilikubaliwa kutumikia kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova, iitwayo Betheli. Nilipowasili huko, nilishangaa kupata kwamba mwanamume mmoja aliyekuwa mkubwa wangu kwa miaka miwili tu, Richard Mucha, alikuwa ndiye mwangalizi wa tawi. Mwaka wa 1955, uhitaji ulipotokea wa watumishi wa mzunguko, kama vile waangalizi wasafirio walivyokuwa wakiitwa wakati huo, nilikuwa miongoni mwa wanaume watano walioalikwa kushiriki katika utumishi huo.

      Mgawo wangu ulikuwa jimbo la Rio Grande do Sul. Kulikuwa na makutaniko 8 tu ya Mashahidi wa Yehova nilipoanza, lakini kabla ya miezi 18 kuisha makutaniko 2 mapya na vikundi 20 vya mbali vilianzishwa. Katika eneo hilo leo, kuna mizunguko 15 ya Mashahidi wa Yehova, kila mmoja ukiwa na makutaniko 20 hivi! Mwishoni mwa mwaka 1956, niliarifiwa kwamba mzunguko wangu ulikuwa umegawanywa kuwa minne midogo ambayo ingetumikiwa na watumishi wanne wa mzunguko. Wakati ule nilielekezwa kurudi Betheli ili kupewa mgawo mpya.

      Kwa mshangao na furaha yangu, nilipewa mgawo kwenda kaskazini mwa Brazili nikiwa mtumishi wa wilaya, mhudumu asafiriye anayetumikia mizunguko kadhaa. Wakati huo Brazili ilikuwa na wahudumu 12,000 wa Mashahidi wa Yehova, na kulikuwa na wilaya mbili nchini. Richard Wuttke alitumikia kusini, nami nilikuwa na wilaya ya kaskazini. Huko Betheli tulizoezwa kutumia projekta ya kuonyesha filamu zilizotokezwa na Mashahidi wa Yehova, The New World Society in Action na The Happiness of the New World Society.

      Siku hizo kusafiri kulikuwa tofauti sana. Hakuna Shahidi aliyekuwa na gari, kwa hiyo tulisafiri kwa mtumbwi, mashua ya kuendeshwa kwa makasia, gari la ng’ombe-dume, farasi, gari la kuburutwa, lori, na wakati mmoja kwa ndege. Ilisisimua kuruka kwa ndege juu ya msitu wa Amazon ili kutua katika Santarém, jiji lililoko kwenye nusu ya njia kati ya Belém kwenye mwanzo wa mto Amazon na Manaus, jiji kuu la Jimbo la Amazonas. Wakati huo watumishi wa wilaya walikuwa na makusanyiko machache ya mizunguko ya kutumikia, kwa sababu hiyo nilitumia wakati wangu mwingi nikionyesha filamu za Sosaiti. Katika majiji makubwa zaidi, mamia ya watu yalihudhuria.

      Jambo lililonivutia zaidi katika kaskazini mwa Brazili lilikuwa ule mkoa wa Amazon. Nilipokuwa nikitumikia huko katika Aprili 1957, Mto Amazon na vijito vyao vilifurika kingo zao. Nilikuwa na pendeleo la kuonyesha mojapo filamu hizo msituni, kwa kunyoosha kati ya miti miwili, kiwambo cha kufanyizwa papo hapo. Nguvu za kuiendesha projekta zilitoka kwenye mashua yenye mota iliyotiwa nanga katika mto ulio karibu. Ilikuwa filamu ya kwanza ambayo walio wengi kati ya wasikilizaji walipata kuona wakati wowote ule.

  • Kumtumikia Yehova Tukiwa Familia Iliyoungana
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Oktoba 1
    • Punde baada ya kurudi Betheli, nilifahamiana na Clara Berndt, tukafunga ndoa Machi 1959. Tulipewa mgawo kufanya kazi ya mzunguko katika jimbo la Bahia, tulimotumikia kwa karibu mwaka mmoja. Clara nami tungali twakumbuka kwa shangwe ule unyenyekevu, ukaribishaji-wageni, bidii, na upendo wa ndugu huko; walikuwa maskini kimwili lakini matajiri katika matunda ya Ufalme. Kisha tukahamishwa hadi Jimbo la São Paulo. Hapo ndipo, mke wangu alipata kuwa mja-mzito mwaka wa 1960, tukalazimika kuacha huduma ya wakati wote.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki