-
Sehemu ya 3—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kadiri hali katika Ulaya zilivyozorota katika 1939, baadhi ya wahudumu mapainia wa Mashahidi wa Yehova walijitolea kutumikia katika mashamba mengine. (Linganisha Mathayo 10:23; Matendo 8:4.) Mapainia watatu kutoka Ujerumani walitumwa kutoka Uswisi hadi Shanghai, China. Idadi fulani yao walienda Amerika Kusini. Miongoni mwa wale waliohamishwa kwenda Brazili alikuwa Otto Estelmann, aliyekuwa amekuwa akitembelea na kusaidia makutaniko katika Chekoslovakia, na Erich Kattner, aliyekuwa ametumikia kwenye ofisi ya Watch Tower Society katika Prague. Mgawo wao mpya haukuwa rahisi. Walipata kwamba, katika sehemu fulani za mashamba, Mashahidi walikuwa wakiamka mapema na kuhubiri hadi saa 1:00 asubuhi na kisha kufanya utumishi zaidi wa shambani wakati wa jioni sana. Ndugu Kattner akumbuka kwamba alipokuwa akitembea toka mahali pamoja hadi pengine, mara nyingi alilala nje, akitumia mkoba wake wa fasihi kama mto.—Linganisha Mathayo 8:20.
Wote wawili Ndugu Estelmann na Ndugu Kattner walikuwa wakiwindwa daima na polisi wa siri wa Nazi katika Ulaya. Je, kuhamia kwao Brazili kuliwaokoa na mnyanyaso? Kinyume cha hivyo, baada ya mwaka mmoja tu, walijipata wakiwa wamezuiliwa nyumbani na kufungwa kwa muda mrefu kwa uchochezi wa maofisa ambao kwa wazi walikuwa marafiki wa Nazi! Upinzani kutoka kwa makasisi Wakatoliki ulikuwa wa kawaida pia, lakini Mashahidi waliendelea na kazi yao waliyopewa na Mungu. Walijitahidi daima kufikia majiji na miji katika Brazili ambayo ujumbe wa Ufalme ulikuwa haujahubiriwa.
-
-
Sehemu ya 3—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 459]
N. H. Knorr (kushoto) kwenye mkusanyiko wa São Paulo katika 1945, Erick Kattner akiwa mkalimani
-