-
Mto Thames—Urithi wa Pekee wa UingerezaAmkeni!—2006 | Februari
-
-
Kabla ya Daraja la Westminster kujengwa katika miaka ya 1740, njia pekee ya kuvuka Mto Thames kwa miguu ilikuwa Daraja la London ambalo lilirekebishwa na baadaye jingine likajengwa mahali pake katika miaka ya 1820. Nguzo zilizotegemeza matao 19 ya daraja la awali zilizuia sana utendaji katika mto huo. Kwa sababu hiyo, katika miaka 600 hivi ya kuwapo kwa daraja hilo, Mto Thames umeganda zaidi ya mara nane hivi. Hilo lilipotendeka, masoko makubwa yalisimamishwa kwenye barafu, ambapo michezo mingi ilifanyiwa. Nyama ya fahali ilichomwa na familia za kifalme zilikula huko. Vitabu na vitu vya kuchezea vilivyokuwa na vibandiko “kimenunuliwa kwenye Mto Thames” vilinunuliwa haraka. Magazeti ya habari na hata nakala za Sala ya Bwana zilichapishwa kwenye matbaa zilizosimamishwa kwenye mto huo ulioganda!
-
-
Mto Thames—Urithi wa Pekee wa UingerezaAmkeni!—2006 | Februari
-
-
[Picha katika ukurasa wa 25]
Daraja la London, lililojengwa kwa mawe, 1756
[Hisani]
From the book Old and New London: A Narrative of Its History, Its People, and Its Places (Vol. II)
-