-
Je, Unafuata “Njia Iliyo Bora Zaidi” Ya Upendo?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
-
-
Si kosa kuwa na rafiki wa karibu katika kutaniko. Hata hivyo, katika 2 Petro 1:7, tunatiwa moyo tuongeze upendo (a·gaʹpe) kwenye ‘upendo wetu wa kindugu’ (phi·la·del·phiʹa, neno linalotokana na maneno mawili, phiʹlos, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “rafiki,” na a·del·phosʹ, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “ndugu”). Ili kufurahia urafiki wa kudumu, tunahitaji kutumia shauri hilo. Tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Je, hisia zangu za urafiki zinasawazishwa na kanuni za Biblia?’
Neno la Mungu linatusaidia kuepuka kuonyesha ubaguzi tunaposhughulika na marafiki wetu. Hatupaswi kutumia viwango viwili tofauti: kiwango kisicho na masharti magumu kwa ajili ya marafiki wetu na kiwango tofauti, chenye masharti magumu kwa ajili ya watu ambao si marafiki wetu. Zaidi ya hayo, hatupaswi kuwasifu-sifu watu au kuwapaka mafuta ili wawe marafiki wetu. Jambo la maana zaidi ni kwamba tunapotumia kanuni za Biblia tunakuwa na utambuzi unaohitajiwa katika kuchagua marafiki na kuepuka ‘mashirika mabaya ambayo yanaharibu tabia nzuri.’—1 Kor. 15:33.
-
-
Je, Unafuata “Njia Iliyo Bora Zaidi” Ya Upendo?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
-
-
Mtume Paulo aliandika hivi: “Upendo wenu na uwe bila unafiki. . . . Katika upendo wa kindugu iweni na upendo mwororo kwa mtu na mwenzake.” (Rom. 12:9, 10) Kwa kweli, Wakristo wana ‘upendo (a·gaʹpe) bila unafiki.’ Upendo huo hautegemei tu hisia inayojitokeza katika mioyo yetu. Badala yake, unategemea kabisa kanuni za Biblia. Hata hivyo, Paulo anataja pia “upendo wa kindugu” (phi·la·del·phiʹa) na “upendo mwororo” (phi·loʹstor·gos, neno linalotokana na maneno phiʹlos na stor·geʹ). Msomi mmoja anasema kwamba “upendo wa kindugu” ni “upendo unaotoka moyoni, unaoonyesha fadhili, huruma, na unaosaidia.” Upendo huo unapounganishwa na a·gaʹpe, unasitawisha uhusiano wa karibu kati ya waabudu wa Yehova. (1 The. 4:9, 10)
-