-
Naweza Kujilinda Jinsi Gani Shuleni?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
Kumshinda Mnyanyasaji Bila Kutumia Ngumi
Wanyanyasaji fulani hutaka tu kukuchokoza waone utafanya nini. Lakini Biblia inatoa shauri hili la hekima: “Usiwe na haraka kuudhika katika roho yako.” (Mhubiri 7:9) Ukweli ni kwamba ‘kulipa uovu kwa uovu’ kunaweza kuongeza kuni kwenye moto na kusababisha matatizo zaidi. (Waroma 12:17) Hivyo basi, unaweza kumshinda jinsi gani mnyanyasaji bila kutumia ngumi?
Usichukulie mambo kwa uzito kupita kiasi. Ikiwa dhihaka imekusudiwa tu kuchekesha, cheka na wengine badala ya kukasirika. Mvulana anayeitwa Eliu anasema: “Nyakati nyingine ni afadhali tu kupuuza maneno ya uchokozi.” Mtu anayekuchokoza akiona kwamba maneno yake hayakuudhi, ataacha kukuchokoza.
Uwe mpole. Biblia inasema: “Jibu, linapokuwa la upole, hugeuza ghadhabu.” (Methali 15:1) Kwa kawaida mnyanyasaji hatazamii kamwe umjibu kwa upole, na kufanya hivyo kunaweza kutuliza hali. Ni kweli kwamba unahitaji kujizuia ili utulie unaposhambuliwa. Sikuzote hilo ndilo jambo linalofaa. Andiko la Methali 29:11 linasema: “Mtu mjinga huiachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima huituliza mpaka mwisho.” Upole si udhaifu. Mtu mpole hapotezi usawaziko kwa urahisi, lakini mara nyingi mnyanyasaji ni mtu ambaye hajiamini, hana kusudi maishani, au amekata tamaa. Ndiyo sababu Biblia inasema: “Asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwanamume mwenye nguvu.”—Methali 16:32.
Jilinde. Hali ikizidi kuwa mbaya, huenda ukahitaji kutafuta ‘njia ya kujitoa’ katika hali hiyo. Andiko la Methali 17:14 linasema: “Kabla mabishano hayajalipuka, jiondokee.” Kwa hiyo, ikiwa unaona kwamba kutakuwa na jeuri, ondoka au hata ukimbie. Ikiwa huwezi kukimbia, unaweza kutumia njia yoyote ili kujikinga.
Ripoti jambo hilo. Wazazi wako wanapaswa kujua kinachotukia. Wanaweza pia kukupa mashauri yanayofaa. Kwa mfano, wanaweza kupendekeza uzungumze na ofisa fulani wa shule, kama vile mshauri, kuhusu jambo hilo. Uwe na hakika kwamba wazazi na walimu wa shule wanaweza kushughulikia hali hiyo kwa busara ili usipate matatizo zaidi.
Tuseme nini basi? Mnyanyasaji hawezi kupata ushindi usipotenda kama anavyotazamia. Hivyo, usikubali kunaswa na mtego wake wa kukufanya ukasirike. Badala yake, unaweza kufanikiwa kwa kutumia mapendekezo yaliyotajwa.
-
-
Naweza Kujilinda Jinsi Gani Shuleni?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
MAANDIKO MUHIMU
“Ikiwezekana, kwa kadiri inavyowategemea ninyi, iweni wenye kufanya amani na watu wote.”—Waroma 12:18.
PENDEKEZO
Ikiwa unanyanyaswa, tenda kwa ujasiri, bali si kwa jeuri. Mwambie anayekunyanyasa akome kabisa. Ondoka bila fujo. Akiendelea, mjulishe mtu anayeweza kukusaidia.
JE, WAJUA . . .?
Kuvaa mavazi ya rangi au mtindo unaotambulisha genge fulani kunaweza kukufanya ushambuliwe. Mtu mmoja aliyeshirikiana na genge fulani anasema: “Ikiwa tungemwona mtu aliyevaa mavazi kama yetu naye si mmoja wetu, kwa kawaida tungemshambulia. Mtu huyo alilazimika kujiunga nasi la sivyo angeona cha mtema-kuni.”
HATUA ZA KUCHUKUA!
Mtu akijaribu kunivunjia heshima au kunichokoza, nita ․․․․․
Ili kujiepusha na matatizo, nita ․․․․․
Mambo ambayo ningependa kuuliza mzazi (wazazi) wangu kuhusu habari hii ․․․․․
UNA MAONI GANI?
● Unaweza kufanya nini ili kuwa na uhakika na utulivu zaidi na hivyo kupunguza uwezekano wa kunyanyaswa?
-
-
Naweza Kujilinda Jinsi Gani Shuleni?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
[Blabu katika ukurasa wa 123]
’Ukijua kwamba vita vitatokea, jiepushe, na uende nyumbani. Wengine hutaka kujionea nao hujikuta katika taabu.’’—Jairo
-
-
Naweza Kujilinda Jinsi Gani Shuleni?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
[Picha katika ukurasa wa 124]
Kutenda kwa hasira unapodhihakiwa na mnyanyasaji ni kama kuongeza mafuta kwenye moto
-