-
Dhuluma Tatizo la Ulimwenguni PoteAmkeni!—2003 | Agosti 22
-
-
Dhuluma Tatizo la Ulimwenguni Pote
“Ukija shuleni kesho, tutakuua.” —Mwanafunzi anayeitwa Kristen huko Kanada alipokea tisho hilo alipopigiwa simu na msichana ambaye hakutaja jina lake.a
“Kwa kawaida siathiriwi sana kihisia, lakini mambo yalizidi kiasi cha kwamba sikutaka kwenda shuleni. Niliumwa na tumbo, na kila asubuhi baada ya kula nilitapika.”—Hiromi, mwanafunzi huko Japan, anaeleza jinsi alivyodhulumiwa.
-
-
Dhuluma Tatizo la Ulimwenguni PoteAmkeni!—2003 | Agosti 22
-
-
Kristen, msichana aliyetajwa mwanzoni, alidhulumiwa na wanafunzi wenzake kwa miaka mingi. Alipokuwa katika shule ya msingi, wanafunzi waliomdhulumu walikuwa wakitia chingamu kwenye nywele zake, walikuwa wakimfanyia mzaha kuhusu sura yake, na kumtisha kwamba wangempiga. Alipokuwa katika shule ya sekondari, mambo yalizidi kiasi cha kwamba alipokea vitisho kupitia simu. Sasa akiwa na umri wa miaka 18, anasema hivi kwa masikitiko: “Mtu huenda shuleni kusoma, bali si kuteswa au kutishwa kwamba atauawa.”
-
-
Dhuluma Tatizo la Ulimwenguni PoteAmkeni!—2003 | Agosti 22
-
-
Dhuluma Iko Ulimwenguni Kote
Ulimwenguni kote watoto wenye umri wa kwenda shule hukabili dhuluma. Uchunguzi uliofanywa na kuchapishwa katika gazeti la Pediatrics in Review ulionyesha kwamba asilimia 14 ya watoto huko Norway huwadhulumu wengine au hudhulumiwa. Nchini Japan, asilimia 15 ya wanafunzi wa shule za msingi wanasema kwamba wao hudhulumiwa, na asilimia 17 hudhulumiwa huko Australia na Hispania. Mtaalamu mmoja anakadiria kwamba watoto milioni 1.3 hudhulumiwa au kuwadhulumu wengine nchini Uingereza.
Profesa Amos Rolider wa Chuo cha Emek Yizre’el aliwahoji wanafunzi 2,972 wa shule 21. Kulingana na gazeti The Jerusalem Post, profesa huyo aligundua kuwa “asilimia 65 walilalamika kwamba walipigwa makofi au mateke, walisukumwa, na kunyanyaswa na wanafunzi wenzao.”
-
-
Dhuluma Baadhi ya Visababishi na MatokeoAmkeni!—2003 | Agosti 22
-
-
Dhuluma Baadhi ya Visababishi na Matokeo
KWA NINI mtoto huanza kuwadhulumu wengine? Ikiwa umewahi kudhulumiwa, huenda ukasema kwamba, “Hata sababu iwe nini hakuna udhuru wa kumdhulumu mwingine.” Na huenda maoni yako ni sawa. Lakini kuna tofauti kubwa kati ya udhuru na sababu. Sababu zinazomfanya mtoto awadhulumu wengine hazifanyi tabia yake mbaya ikubalike, lakini zinaweza kutusaidia kuielewa. Na ni muhimu sana kuelewa kwa nini anatenda hivyo. Kwa nini?
Methali moja ya kale inasema hivi: “Ufahamu wa mtu hakika hupunguza hasira yake.” (Mithali 19:11, NW) Tukikasirishwa na tabia ya mdhalimu tunaweza kukata kauli kimakosa, na hivyo kufadhaika sana na hata kumchukia. Lakini tukiielewa tabia yake tunaweza kupunguza hasira yetu. Hilo linaweza kutusaidia kuwa na maoni yanayofaa tunapotafuta masuluhisho. Kwa hiyo, hebu tuchunguze visababishi kadhaa vya tabia hiyo mbaya.
Kwa Nini Watu Huwadhulumu Wengine?
Wadhalimu wengi huiga mfano mbaya wa wazazi wao au walipuuzwa kabisa na wazazi wao walipokuwa watoto. Wengi wana wazazi ambao si wachangamfu, wasiojali, au ambao wamewawekea watoto wao mfano mbaya kwa kushughulikia matatizo kwa hasira na jeuri. Huenda watoto ambao wamelelewa kwa njia hiyo wasione kwamba wanawadhulumu wengine kwa maneno na matendo yao ya jeuri. Huenda hata wakafikiri kwamba tabia yao ni sawa kabisa.
Msichana mmoja mwenye umri wa miaka 16 ambaye alidhulumiwa na baba yake wa kambo na vilevile na wanafunzi wenzake shuleni, alibadilika kuwa mdhalimu alipofika darasa la saba. Anasema hivi: “Nilikuwa na hasira nyingi; nilimdhulumu mtu yeyote tu. Kuhisi uchungu si jambo dogo. Mtu anapoumizwa, yeye hutaka kuwaumiza wengine pia.” Ijapokuwa kwa kawaida wasichana wanaowadhulumu wengine hawatumii jeuri, wao huwadhulumu wengine kwa sababu wamekasirika.a
Shule nyingi huwa na wanafunzi wengi ambao wamelelewa kwa njia zinazotofautiana sana. Kwa kusikitisha, watoto fulani huwa wajeuri kwa sababu wamefundishwa nyumbani kwamba kuwatisha wengine na kuwatusi ndizo njia bora za kupata wanachotaka.
Inasikitisha kwamba mara nyingi njia hizo hufaulu. Shelley Hymel, ambaye ni mshauri msaidizi kwenye Chuo Kikuu cha British Columbia, Kanada, amechunguza tabia za watoto kwa miaka ishirini. Anasema hivi: “Kuna watoto ambao wanajua jinsi ya kupata wanachotaka, na inasikitisha kwamba wao hufanikiwa wanapowadhulumu wengine. Wao hufaulu kupata wanachotaka, yaani, wanapata mamlaka, hadhi na umashuhuri.”
Ukosefu wa mwongozo ni jambo jingine linalofanya dhuluma iongezeke. Watu wengi wanapodhulumiwa huhisi kwamba hakuna mtu anayeweza kuwasaidia na inasikitisha kwamba hali huwa hivyo mara nyingi. Debra Pepler, mkurugenzi wa Kituo cha LaMarsh cha Utafiti Kuhusu Jeuri na Masuluhisho ya Ugomvi kwenye Chuo Kikuu cha York huko Toronto, alifanya uchunguzi kuhusu wanafunzi wa shule na akagundua kwamba walimu hutambua na kukomesha karibu asilimia 4 tu ya visa vya dhuluma.
Hata hivyo, Dakt. Pepler anaamini kwamba ni muhimu kukomesha hali hiyo. Anasema hivi: “Watoto hawawezi kutatua tatizo hilo kwa sababu linahusu nguvu, na mdhalimu hupata nguvu zaidi kila mara anapomdhulumu mtu.”
Kwa hiyo, kwa nini visa vingi vya dhuluma haviripotiwi? Ni kwa sababu wale wanaodhulumiwa huamini kwamba wakiripoti jambo hilo, huenda mambo yakawa mabaya zaidi. Hivyo, vijana wengi huwa na wasiwasi kwa kadiri fulani na hukosa usalama katika miaka yao ya shule. Ni nini matokeo ya hali hiyo?
Athari za Kimwili na Kihisia
Ripoti ya shirika moja la wataalamu wa akili huko Marekani inasema kwamba kila siku zaidi ya watoto 160,000 hukosa kwenda shule kwa sababu wanaogopa kudhulumiwa. Huenda wale wanaodhulumiwa wakaacha kuzungumza juu ya shule au juu ya somo fulani au shughuli fulani hususa ya shuleni. Huenda wakajaribu kuchelewa kwenda shuleni kila siku au kuhepa masomo fulani au hata kutoa udhuru ili wasiende shuleni.
Watoto wanaodhulumiwa wanaweza kutambuliwaje? Huenda wakanuna, wakakasirika haraka, wakavunjika moyo, wakaonekana wachovu, au wakajitenga. Wanaweza kuwadhulumu watoto wenzao nyumbani au marafiki zao. Watoto wanaoshuhudia wengine wakidhulumiwa huathiriwa pia. Hali hiyo huwaogopesha sana na hudhoofisha uwezo wao wa kujifunza.
Hata hivyo, gazeti Pediatrics in Review lasema hivi: “Tokeo baya zaidi la dhuluma miongoni mwa wale waliodhulumiwa na katika jamii ni jeuri, na hiyo inatia ndani kujiua na kuwaua wengine. Watoto wanaodhulumiwa huhisi kwamba hawana nguvu kabisa hivi kwamba wengine wao huamua kujiua au kuwaua wengine.”
Dakt. Ed Adlaf, mtafiti na profesa wa afya ya umma kwenye Chuo Kikuu cha Toronto, anasema kuwa “kuna uwezekano mkubwa kwamba wadhalimu au wanaodhulumiwa wataumia kihisia sasa na baadaye.” Katika mwaka wa shule wa 2001, zaidi ya wanafunzi 225,000 huko Ontario walihojiwa, na kati ya robo na thuluthi ya wanafunzi hao walidhulumiwa au kuwadhulumu wengine. Mwanafunzi 1 kati ya 10 alikuwa amefikiria sana kujiua.
Mtu anapodhulumiwa sana anaweza kuacha kujiamini, kupatwa na magonjwa hatari, na hata kushindwa kuendelea na kazi. Huenda watu wanaodhulumiwa wakaumwa na kichwa, wakakosa usingizi, wakawa na wasiwasi, na hata kushuka moyo. Wengine hupata ugonjwa fulani unaosababishwa na mfadhaiko. Ijapokuwa mtu anapoumizwa kimwili anaweza kuhurumiwa sana, mambo huwa tofauti anapoumizwa kihisia. Watu hawawezi kujua kwa urahisi kwamba anaumia. Kwa hiyo badala ya kumhurumia, huenda marafiki na watu wa familia wakachoshwa na malalamiko yake.
Wadhalimu pia huathiriwa na dhuluma. Wasipokomeshwa wanapokuwa wadogo, huenda wakawadhulumu wafanyakazi wenzao wanapokuwa watu wazima. Miradi fulani ya uchunguzi inaonyesha kwamba watu waliokuwa wadhalimu walipokuwa watoto walikuwa na tabia hiyohiyo hata walipokuwa watu wazima. Pia, kuna uwezekano mkubwa kwamba watakuwa wahalifu.
-