Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usijitenge Kamwe na Waamini Wenzako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Machi 15
    • Usijitenge Kamwe na Waamini Wenzako

      “KWA miaka kumi, tulisisimuliwa na mambo yenye kuvutia katika ulimwengu wa biashara, na tulikuwa matajiri sana. Ingawa tulilelewa katika kweli, tulikuwa tumejitenga kabisa na Yehova na hatukuwa na nguvu za kiroho za kurudi,” anasema Jarosław na mke wake, Beata.a

      Ndugu mwingine anayeitwa Marek, anakumbuka hivi: “Kwa sababu ya mabadiliko ya kijamii na kisiasa nchini Poland, nilipoteza kazi mara nyingi. Nilivunjika moyo. Niliogopa kuanzisha kampuni yangu mwenyewe kwa sababu sikuwa na uwezo au kipawa cha kufanya biashara. Mwishowe, nilishawishiwa kuanzisha kampuni yangu, huku nikifikiri kwamba jambo hilo lingenisaidia kutosheleza vizuri zaidi mahitaji ya kimwili ya familia yangu bila kupata matatizo yoyote ya kiroho. Baada ya muda, niligundua kwamba nilikuwa nimekosea kabisa.”

  • Usijitenge Kamwe na Waamini Wenzako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Machi 15
    • Kulemewa na Mahangaiko ya Maisha

      Kama tulivyoona, kufanya kazi kwa bidii ili kutosheleza mahitaji ya msingi ya familia mara nyingi kunasababisha mahangaiko na kunaweza kutufanya tupuuze mambo ya kiroho. (Mt. 13:22) Marek, aliyetajwa mwanzoni, anaeleza hivi: “Biashara yangu ilipoporomoka, niliamua kutafuta kazi yenye mshahara mnono katika nchi za nje. Nilienda huko kwa miezi mitatu tu, kisha nikaongeza miezi mingine mitatu, na kadhalika, na nilirudi nyumbani mara kwa mara. Mke wangu ambaye si mwamini aliteseka kihisia kwa sababu hiyo.”

      Maisha ya familia na pia mambo mengine yaliharibika. Marek anaendelea kusema: “Nilifanya kazi kwa saa nyingi katika joto kali sana, na zaidi ya hayo, nilifanya kazi na watu waliotumia lugha chafu ambao walijitahidi kuwakandamiza wengine. Walitenda kama majambazi. Nilishuka moyo na kuhisi nimelemewa. Sikuwa hata na wakati wa kujitunza mwenyewe, nilianza kutilia shaka uwezo wangu wa kuwatumikia wengine.”

  • Usijitenge Kamwe na Waamini Wenzako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Machi 15
    • Hata hivyo, huenda unatambua kwamba mtu anaweza kujishughulisha sana na kazi ya kimwili hata kama hafanyi kazi katika nchi nyingine. Mfikirie Jarosław na Beata. Jarosław anasema hivi: “Tulianza kwa unyoofu kabisa. Tukiwa wenzi wapya wa ndoa, tulifungua duka dogo katika eneo zuri ili kuuza soseji zinazotiwa katika mikate. Tulipata faida kubwa sana ambayo ilituchochea kupanua biashara yetu. Lakini hatukuwa na wakati wa kutosha, kwa hivyo tulikosa mikutano ya Kikristo. Baada ya muda mfupi, niliacha upainia na pia nikaacha kutumika nikiwa mtumishi wa huduma. Tulisisimuka sana kwa sababu ya faida kubwa ambayo tulikuwa tukipata hivi kwamba tulifungua duka kubwa tukishirikiana na mtu asiye mwamini. Baada ya muda, nilikuwa nikisafiri nchi za nje ili kutia sahihi mapatano ya kibiashara yenye thamani ya mamilioni ya dola. Kwa kawaida sikupatikana nyumbani, na uhusiano wangu na mke wangu na pia binti yangu uliharibika. Mwishowe, tulijishughulisha sana na biashara hiyo iliyokuwa ikisitawi hivi kwamba tuliacha kumtumikia Yehova hatua kwa hatua. Baada ya kujitenga na kutaniko, hatukuwafikiria hata kidogo ndugu zetu.”

  • Usijitenge Kamwe na Waamini Wenzako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Machi 15
    • Katika muda wa miaka michache, wazee wenye upendo walijitahidi kumjenga na kumtia moyo Jarosław. Alichochewa kufanya mabadiliko makubwa katika maisha yake. Anasema hivi: “Pindi moja tulipokuwa na mazungumzo yenye kugusa moyo, wazee walitaja mfano wa Kimaandiko wa kijana mmoja tajiri ambaye alitaka kuishi milele lakini hakuwa tayari kuacha vitu vyake vya kimwili. Kisha wazee hao wakaniuliza kwa busara ikiwa habari hiyo inanihusu. Jambo hilo lilinifungua macho nikaona marekebisho niliyohitaji kufanya!”—Met. 11:28; Marko 10:17-22.

      Jarosław alichunguza kwa unyoofu hali yake akaamua kuacha kujishughulisha na biashara kubwa. Katika muda wa miaka miwili, yeye na familia yake walirudia hali yao nzuri ya kiroho. Sasa anawatumikia ndugu zake akiwa mzee. Jarosław anasema hivi: “Ndugu wanapojishughulisha sana na mambo ya kibiashara na kupuuza hali yao ya kiroho, ninatumia mfano wangu kuwaonyesha kwamba si jambo la hekima kufungwa nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini. Si rahisi kushinda vishawishi vyenye kuvutia na kuepuka mazoea yasiyo ya unyoofu.”—2 Kor. 6:14.

      Marek pia alijifunza somo fulani kwa njia ngumu. Ingawa alipata kazi yenye mshahara mnono katika nchi ya nje ambayo ilisaidia familia yake kifedha, uhusiano wake pamoja na Mungu na ndugu zake uliharibika. Baada ya muda, alibadili mambo ambayo alikuwa akitanguliza. “Kwa miaka mingi, hali yangu ilikuwa kama ya Baruku wa zamani ambaye ‘aliendelea kujitafutia makuu.’ Mwishowe, nilifunua moyo wangu, nikamwambia Yehova mahangaiko yangu, na sasa ninahisi kwamba nimepata tena usawaziko wa kiroho.” (Yer. 45:1-5) Sasa Marek anajitahidi kufikia “kazi njema” ya kuwa mwangalizi katika kutaniko.—1 Tim. 3:1.

      Marek anawaonya hivi wale ambao huenda wanafikiria kwenda nchi za nje ili kutafuta kazi yenye mshahara mnono: “Ukiwa katika nchi ya nje, ni rahisi sana kuanguka katika mitego ya ulimwengu huu mwovu. Kutojua vizuri lugha ya wenyeji kunakuzuia kuwasiliana na wengine. Huenda ukarudi nyumbani ukiwa na pesa, lakini pia unapata vidonda vya kiroho ambavyo vinaweza kuchukua muda mrefu kupona.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki