Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • 4. Wakristo fulani huamua kufanya arusi ya aina gani, na kwa nini?

      4 Katika nchi nyingi leo, ni lazima Wakristo wanaotaka kufunga ndoa watimize matakwa fulani ya kisheria. Baada ya kuyatimiza, wanaweza kufanya arusi kwa njia yoyote inayokubalika kisheria. Wanaweza kufuata utaratibu usiohusisha mambo mengi, wakisimamiwa na hakimu, meya, au mhudumu aliyepewa mamlaka na Serikali. Watu fulani huamua kufanya arusi kwa njia hiyo, labda kwa kuwaalika watu wachache wa ukoo au marafiki Wakristo ili wawe mashahidi wa kisheria au washiriki shangwe ya tukio hilo muhimu. (Yeremia 33:11; Yohana 3:29)

  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • Ndoa Inayoheshimika Ni Ndoa Halali Kisheria

      6, 7. Kwa nini tunapaswa kutilia maanani matakwa ya kisheria kuhusu kufunga ndoa, nasi tunaweza kuonyeshaje kwamba tunafanya hivyo?

      6 Ingawa Yehova alianzisha ndoa, serikali za wanadamu zimeweka sheria fulani kwa wale wanaofunga ndoa. Na hilo ni jambo linalofaa. Yesu alisema: “Mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.” (Marko 12:17) Vivyo hivyo, mtume Paulo alitoa mwongozo huu: “Kila nafsi na ijitiishe kwa mamlaka zilizo kubwa, kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kwa njia ya Mungu; mamlaka zilizopo zimesimamishwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.”—Waroma 13:1; Tito 3:1.

      7 Katika nchi nyingi, Kaisari, au serikali, huamua ni nani anayestahili kufunga ndoa. Kwa hiyo, Wakristo wawili ambao wako huru Kimaandiko wanapoamua kufunga ndoa, wanajitahidi kufuata sheria za nchi yao kuhusu ndoa. Huenda sheria hizo zikatia ndani kupata cheti cha ndoa, kutumia ofisa aliyewekwa rasmi na serikali, na labda kuiandikisha ndoa. Kaisari Agusto alipoagiza watu wakafanye “uandikisho,” Maria na Yosefu walitii agizo hilo, nao wakaenda Bethlehemu ‘ili wapate kuandikishwa.’—Luka 2:1-5.

      8. Mashahidi wa Yehova hawafanyi nini, na kwa nini?

      8 Wakristo wawili wanapofunga ndoa kupatana na matakwa ya kisheria yanayokubalika, wanakuwa na wajibu machoni pa Mungu. Hivyo, Mashahidi wa Yehova hawaandikishi ndoa mara ya pili kwa kurudia utaratibu wa kisheria, wala hawarudii nadhiri za ndoa, kama vile wakati wenzi wanapoadhimisha mwaka wa 25 au 50 wa arusi yao. (Mathayo 5:37) (Makanisa fulani hupuuza utaratibu wa ndoa ya kiserikali, yakidai kwamba si ndoa halali kwa sababu kasisi au kiongozi wa dini hakufanya sherehe au kuwatangaza kuwa mume na mke.) Katika nchi nyingi, serikali humpa mhudumu wa Mashahidi wa Yehova mamlaka ya kuandikisha ndoa. Ikiwa ndivyo ilivyo, yaelekea kwamba atafanya hivyo katika Jumba la Ufalme ambapo hotuba ya arusi itatolewa. Jumba la Ufalme ni mahali pa ibada ya kweli na panafaa kwa ajili ya hotuba inayohusu mpango huo ambao ulianzishwa na Yehova Mungu.

      9. (a) Wakristo wanaotaka kufunga ndoa ya kiserikali, wanaweza kuamua kufanya nini? (b) Wazee wanaweza kuhusikaje katika mipango ya arusi?

      9 Kulingana na sheria za nchi nyingine, watu wanahitajiwa kufunga ndoa katika ofisi za serikali, kama vile makao makuu ya halmashauri ya jiji, au mbele ya ofisa aliyewekwa rasmi na serikali. Mara nyingi, baada ya kuchukua hatua hiyo ya kisheria, Wakristo huamua kuwa na hotuba ya arusi kwenye Jumba la Ufalme siku hiyohiyo au siku inayofuata.

  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • 11. Katika nchi fulani, mwanamume na mwanamke hufungaje ndoa, na ni mambo gani yatakayotajwa katika hotuba ya arusi?

      11 Katika nchi fulani, huenda sheria isiruhusu mwanamume na mwanamke wafunge ndoa kwa kufuata utaratibu fulani rasmi, hata mbele ya ofisa wa serikali. Arusi hutukia wakati wanapompa ofisa cheti cha ndoa kilichotiwa sahihi. Mara tu baada ya hapo, cheti hicho cha ndoa huandikishwa. Katika njia hiyo, mwanamume na mwanamke huonwa kuwa mume na mke, na siku hiyo kuwa tarehe ya ndoa yao. Kama ilivyotajwa mwanzoni, huenda wenzi hao waliofunga ndoa wakaamua kwamba hotuba inayotegemea Biblia itolewe kwenye Jumba la Ufalme.

  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • Ndoa ya Kimila na ya Kiserikali

      12. Ndoa ya kimila ni ndoa ya aina gani, na wale walio katika ndoa hiyo wanapaswa kufanya nini?

      12 Katika nchi fulani, huenda wale wanaotaka kufunga ndoa wakaamua kufanya ndoa ya kimila. Hilo halirejelei watu wawili wanaoishi tu pamoja, wala halirejelei wale wanaoishi pamoja kama mume na mke kwa njia isiyo halali. Huenda zoea hilo likakubaliwa katika maeneo mengine ingawa si ndoa halali kabisa.d Tunazungumzia ndoa ambayo inafuata desturi zinazotambuliwa na wengi katika kabila au eneo fulani. Huenda hilo likatia ndani kulipa kabisa na kukubaliwa kwa mahari, na hivyo wenzi hao wanakuwa wamefunga ndoa halali kisheria na Kimaandiko. Serikali huona ndoa hiyo ya kimila kuwa halali kisheria na isiyoweza kuvunjwa. Kwa kawaida, ndoa hiyo ya kimila inaweza baadaye kuandikishwa na wenzi kupewa cheti rasmi. Kuandikisha ndoa kunaweza kuwa ulinzi kwa wenzi hao au kwa mke ikiwa atakuwa mjane na kwa watoto wowote ambao huenda wakazaliwa baadaye. Kutaniko linapaswa kumhimiza yeyote ambaye amefanya ndoa ya kimila aiandikishe haraka iwezekanavyo. Inaonekana kwamba chini ya Sheria ya Musa, ndoa na kuzaliwa kwa watoto kuliandikishwa kirasmi.—Mathayo 1:1-16.

      13. Baada ya kufunga ndoa ya kimila, hotuba ya arusi inafaa ishughulikiweje?

      13 Wenzi waliounganishwa kwa njia halali katika ndoa ya kimila wanakuwa mume na mke wanapofunga ndoa hiyo.

  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • 14. Mkristo anaweza kufanya nini ikiwa ndoa za kimila na kiserikali zinakubalika?

      14 Katika nchi fulani ambako ndoa za kimila zinaonwa kuwa ndoa halali, kuna pia ndoa za kiserikali (au kisheria). Kwa kawaida, ndoa za kiserikali hufungwa mbele ya ofisa wa serikali, na huenda zikahusisha kuweka nadhiri ya ndoa na kutia sahihi cheti. Wakristo fulani wanapendelea ndoa za kiserikali badala ya ndoa za kimila. Si takwa la kisheria kufuata taratibu zote mbili; kila moja ya ndoa hizo ni halali kisheria.

  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • 17. Kwa nini arusi za Kikristo huhusisha matakwa ya kisheria?

      17 Yaelekea kwamba umeona makala hii ina mambo mengi ya kisheria kuhusu ndoa. Huenda baadhi ya mambo hayo yasihusu eneo lenu moja kwa moja. Hata hivyo, sote tunapaswa kutambua kwamba ni muhimu mipango ya arusi miongoni mwa Mashahidi wa Yehova ipatane na sheria za nchi na matakwa ya Kaisari. (Luka 20:25) Paulo alituhimiza hivi: “Wapeni wote haki zao, yeye anayetaka kodi, kodi; yeye anayetaka ushuru, ushuru; yeye anayetaka . . . heshima, heshima hiyo.” (Waroma 13:7) Naam, inafaa Wakristo, tangu siku ya arusi, waheshimu mpango wa Mungu uliopo sasa wa ndoa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki