-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2002 | Agosti 1
-
-
Kwa hiyo, Mungu alikubali dhabihu ya Abeli lakini akakataa ya Kaini. Kwa nini? Je, ni kwa sababu Abeli alitoa dhabihu inayofaa naye Kaini akatoa isiyofaa? Hatuwezi kuwa na uhakika kwamba aina ya dhabihu walizotoa ndizo zilizomfanya Mungu akubali moja na kukataa nyingine kwa kuwa hawakuwa wameambiwa ni dhabihu za aina gani zinazokubalika na zisizokubalika. Hata hivyo, yaelekea kwamba dhabihu walizotoa zilikubalika. Katika Sheria ambayo mwishowe Yehova alilipa taifa la Israeli, dhabihu zilizokubalika zilitia ndani wanyama, sehemu za wanyama, na pia nafaka iliyochomwa, miganda ya shayiri, unga mwembamba, vitu vilivyookwa, na divai. (Mambo ya Walawi 6:19-23; 7:11-13; 23:10-13) Yaonekana kwamba si vitu walivyotoa tu vilivyofanya Mungu akubali dhabihu ya Abeli na kukataa ya Kaini.—Linganisha Isaya 1:11; Amosi 5:22.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2002 | Agosti 1
-
-
Vivyo hivyo, Kaini alikataliwa kwa sababu alikosa imani, kama matendo yake yalivyoonyesha, bali si kwa sababu alitoa dhabihu isiyofaa. Yehova alikuwa amemweleza Kaini waziwazi hivi: “Kama ukitenda vyema, hutapata kibali?” (Mwanzo 4:7) Mungu hakumkataa Kaini kwa sababu alichukizwa na dhabihu yake, bali alimkataa kwa sababu “kazi zake mwenyewe zilikuwa mbovu.” Kaini alikuwa mwenye wivu, chuki, na hatimaye akawa mwuaji.—1 Yohana 3:12.
-