-
Kumtolea Yehova Dhabihu Zenye KukubalikaMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 1
-
-
Tofauti na Abeli, Kaini alitoa “mazao ya ardhi.” Yehova aliikubali dhabihu ya Abeli, bali “Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake.” (Mwanzo 4:3-5) Kwa nini?
Wengine huonyesha uhakika wa kwamba dhabihu ya Abeli ilitokana na “wazao wa kwanza wa wanyama wake,” ilhali ya Kaini ilikuwa tu “mazao ya ardhi.” Lakini tatizo halikuwa ubora wa mazao ambayo Kaini alitoa, kwa kuwa simulizi hilo lasema kwamba Yehova alimtakabali ‘Abeli na sadaka yake,’ bali “Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake.” Kwa hiyo, Yehova alitazama hasa hali ya moyo ya mwabudu huyo. Ni nini alichotambua kwa kufanya hivyo? Andiko la Waebrania 11:4 lasema kwamba Abeli alitoa dhabihu yake “kwa imani.” Kwa hiyo, yaonekana dhabihu ya Kaini ilikosa imani iliyofanya dhabihu ya Abeli ikubaliwe.
-
-
Kumtolea Yehova Dhabihu Zenye KukubalikaMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 1
-
-
Tofauti na hilo, yaelekea Kaini alifikiria kijuujuu tu dhabihu aliyotoa. “Dhabihu yake ilikuwa tu ishara ya kumtambua Mungu kuwa mfadhili,” akadokeza mwelezaji mmoja wa Biblia wa karne ya 19. “Ilifunua waziwazi kwamba hakutambua kuvunjika kokote halisi kwa uhusiano kati yake na Muumba wake, wala uhitaji wowote wa kutubu dhambi au kutegemea ufuniko fulani.”
Isitoshe, akiwa mzaliwa wa kwanza, huenda Kaini hata alidhania kwa kiburi kwamba yeye ndiye mbegu aliyeahidiwa ambaye angemharibu Nyoka, Shetani. Yawezekana Hawa pia alikuwa na tamaa hiyo kubwa ya makuu kwa ajili ya mwana wake wa kwanza. (Mwanzo 4:1) Bila shaka, ikiwa hivyo ndivyo Kaini na Hawa walivyotarajia, walikuwa wamekosea sana.
-