-
Waliboresha Maisha Yao—Je, Unaweza Kuwaiga?Mnara wa Mlinzi—2008 | Januari 15
-
-
Waliboresha Maisha Yao—Je, Unaweza Kuwaiga?
MARC, ndugu fulani nchini Kanada, aliajiriwa kazi na kampuni fulani ya kutengeneza roboti za hali ya juu zinazotumiwa na mashirika ya anga za juu. Alikuwa akifanya kazi ya muda na pia alikuwa painia wa kawaida. Kisha, msimamizi fulani akampa Marc nafasi ya kupandishwa cheo—kazi ya siku nzima na mshahara mkubwa. Marc alifanya nini?
-
-
Waliboresha Maisha Yao—Je, Unaweza Kuwaiga?Mnara wa Mlinzi—2008 | Januari 15
-
-
“Tunajihisi Tukiwa Karibu Zaidi na Yehova Kuliko Zamani”
Marc, aliyetajwa mwanzoni, alitii shauri la Biblia kuhusu kutotumia ulimwengu kwa ukamili. Alikataa cheo kikubwa alichopewa kazini. Siku chache baadaye, msimamizi wake alimwahidi mshahara mnono hata zaidi ili kumshawishi akubali cheo hicho. “Hilo lilikuwa jaribu,” anasema Marc, “lakini nilikataa tena.” Anaeleza kwa nini alikataa: “Mimi na mke wangu Paula, tulitaka utumishi kwa Yehova uwe jambo kuu iwezekanavyo maishani mwetu. Hivyo, tuliazimia kurahisisha maisha yetu. Tulimwomba Yehova atupe hekima ili tufikie mradi wetu na tukaweka tarehe hususa tuliyotaka kuanza kumtumikia Yehova kwa kadiri kubwa zaidi.”
Paula anasema hivi: “Nilifanya kazi siku tatu kwa juma nikiwa mwandishi katika hospitali fulani nami nilipokea mshahara mzuri. Pia nilikuwa painia wa kawaida. Hata hivyo, kama Marc, mimi pia nilitaka kumtumikia Yehova mahali popote penye uhitaji mkubwa zaidi wa watangazaji wa Ufalme. Lakini, nilipopeleka ombi langu la kujiuzulu, msimamizi wangu alisema ninastahili kuwa katibu mkuu, nafasi iliyokuwa tu imetokea. Hicho kilikuwa cheo chenye mshahara mkubwa zaidi cha katibu katika hospitali hiyo, lakini nilishikamana na uamuzi wangu wa kujiuzulu. Nilipomweleza msimamizi huyo kwa nini ninakataa cheo hicho, alinipongeza kwa sababu ya imani yangu.”
Muda mfupi baadaye, Marc na Paula walipokea mgawo wa kutumika wakiwa mapainia wa pekee katika kutaniko dogo katika eneo la mbali huko Kanada. Walipata matokeo gani kwa kuhamia eneo hilo? Marc anasema: “Nilikuwa na wasiwasi baada ya kuacha kazi yenye kutegemeka ambayo nilikuwa nimefanya karibu nusu ya maisha yangu, lakini Yehova alibariki huduma yetu. Tuna shangwe kubwa sana inayotokana na kuwapa wengine zawadi za kiroho. Pia, utumishi wa wakati wote umeboresha ndoa yetu. Mazungumzo yetu yanahusu mambo yaliyo ya maana kikweli, mambo ya kiroho. Tunajihisi tukiwa karibu zaidi na Yehova kuliko zamani.” (Mdo. 20:35) Paula anaongezea: “Unapoacha kazi yako na starehe za nyumbani, unalazimika kumtegemea Yehova kabisa. Tulifanya hivyo, na Yehova akatubariki. Ndugu na dada wapendwa katika kutaniko letu jipya wanatufanya tuhisi tunapendwa na kuhitajiwa. Sasa ninatumia nguvu nilizokuwa nikitumia kazini kuwasaidia watu kiroho. Ninashangilia sana kutumika katika mgawo huu.”
-