-
Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
VISIWA vingi vya Indies Magharibi vilikuwa vimefikiwa kwa njia fulani kwa ujumbe wa Ufalme kufikia 1945. Lakini ushahidi kamili zaidi ulihitaji kutolewa. Wamishonari waliozoezwa kwenye Shule ya Gileadi wangetimiza fungu la maana.
Wamishonari Wazidisha Ushahidi Katika Indies Magharibi
Kufikia 1960 wamishonari hao walikuwa wametumikia katika visiwa au vikundi vya visiwa 27 katika Karibea. Nusu ya sehemu hizo hazikuwa na kutaniko la Mashahidi wa Yehova wakati wamishonari walipowasili. Wamishonari walianza na wakaendelea kuongoza mafunzo ya Biblia nyumbani pamoja na watu wenye kupendezwa, na wakapanga mikutano ifanywe kwa ukawaida. Mahali ambako tayari kulikuwa makutaniko, walitoa mazoezi muhimu kwa wahubiri wenyeji. Kama tokeo, kulikuwa na maendeleo katika ubora wa mikutano na mafanikio katika huduma.
Wale Wanafunzi wa Biblia wa mapema walikuwa wametoa ushahidi katika Trinidad tangu kabla ya Vita ya Ulimwengu 1, lakini kufuatia kuwasili kwa wamishonari kutoka Gileadi katika 1946, kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia nyumbani na watu wenye kupendezwa ilipewa nguvu mpya. Katika Jamaika kazi ya kuhubiri habari njema ilikuwa imeanza muda wa karibu nusu karne, na kulikuwa Mashahidi wenyeji elfu moja kufikia wakati wamishonari wa kwanza walipowasili; lakini walifurahi kusaidiwa kufikia watu wenye elimu zaidi, hasa katika sehemu za viunga kuzunguka jiji kuu. Kwa upande mwingine, katika Aruba kazi nyingi ya kutoa ushahidi ilikuwa tayari imefanywa katika jamii ya wenye kusema Kiingereza, hivyo wamishonari walielekeza fikira zao kwa wenyeji. Kila mtu alihitaji kusikia habari njema.
Ili kuhakikisha kwamba watu katika visiwa vyote katika sehemu hiyo ya dunia walikuwa na fursa ya kusikia juu ya Ufalme wa Mungu, katika 1948 Watch Tower Society ilitayarisha ile mashua Sibia yenye urefu wa meta 18 kuwa makao ya wamishonari yenye kuelea. Kikundi cha wafanyakazi kilipewa mgawo kupeleka ujumbe wa Ufalme kwenye kila kisiwa cha Indies Magharibi ambacho hakikuwa na yeyote akifanya kazi ya kuhubiri habari njema. Gust Maki alikuwa ndiye kapteni, na waliokuwa pamoja naye ni Stanley Carter, Ronald Parkin, na Arthur Worsley. Walianza na Visiwa Out vya kikundi cha Bahamas, kisha wakafanya kazi kuelekea kusini-mashariki kupitia Visiwa vya Leeward na Visiwa vya Windward. Ziara zao zilikuwa na matokeo gani? Katika St. Maarten mfanyabiashara mmoja aliwaambia hivi: “Watu hawakuzoea kamwe kuongea juu ya Biblia, lakini tangu mwe hapa kila mtu anaongea juu ya Biblia.” Baadaye, mahali pa Sibia palichukuliwa na mashua kubwa zaidi, Light. Pia kulikuwa badiliko katika wafanyakazi. Katika muda wa mwongo mmoja kazi hiyo ya pekee iliyokuwa ikifanywa kwa kutumia mashua hizo ikawa imekamilishwa, nao wapiga-mbiu wa habari njema wakaao kwenye nchi kavu walikuwa wakifuatia kupendezwa.
-
-
Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Ramani/Picha katika ukurasa wa 462]
Mashua “Sibia” ilitumika kuwa kao la kimishonari lenye kuelea katika Indies Magharibi
G. Maki
S. Carter
R. Parkin
A. Worsley
-