-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na baada ya siku tatu na nusu roho ya uhai kutoka kwa Mungu iliingia ndani yao, na wao wakasimama kwa nyayo zao, na hofu kubwa ikaanguka juu ya wale waliokuwa wakiona wao.
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
24. Mashahidi wawili walipokuja kwenye uhai tokeo lilikuwa nini kwa wanyanyasi wao wa kidini?
24 Ulikuwa mshtuko kama nini kwa wanyanyasi hao! Ghafula maiti za mashahidi wawili zikawa hai tena na zenye kutenda. Viongozi wa kidini hao waliona uchungu sana, na zaidi hivyo kwa kuwa wahudumu hao Wakristo ambao walikuwa wametungia hila wawaweke katika gereza walikuwa huru tena, na baadaye wakaondolewa mashtaka kabisa. Mshtuko huo lazima uwe ulikuwa mkubwa hata zaidi wakati, katika Septemba 1919, hao Wanafunzi wa Biblia walipofanya mkusanyiko katika Sida Pointi Ohaiyo, U.S.A. Huko J. F. Rutherford, aliyeachiliwa karibuni, alichochea wakusanyikaji kwa hotuba yake “Kutangaza Ufalme,” iliyotegemea Ufunuo 15:2 na Isaya 52:7. Wale wa jamii ya Yohana wakaanza tena ‘kutoa unabii,’ au kuhubiri peupe. Walizidi kupata imara tena na tena, wakifichua kwa ujasiri unafiki wa Jumuiya ya Wakristo.
-