-
Useja—Mlango Uelekeao Kwenye Utendaji Pasipo Kukengeushwa FikiraMnara wa Mlinzi—1996 | Oktoba 15
-
-
Hakuna Nadhiri ya Useja wa Daima
21. (a) Kwa nini ni wazi kwamba Paulo hakutia moyo kuweka nadhiri ya useja? (b) Alidokeza nini aliposema juu ya ‘kupita mchanuko wa ujana’?
21 Jambo kuu katika shauri la Paulo ni kwamba Wakristo wangefanya “vema” kufanyia nafasi useja maishani mwao. (1 Wakorintho 7:1, 8, 26, 37) Hata hivyo, yeye hawaaliki kwa vyovyote waweke nadhiri ya useja. Kinyume cha hilo, aliandika hivi: “Ikiwa yeyote afikiri anajiendesha isivyofaa kuelekea ubikira wake, ikiwa huo umepita mchanuko wa ujana, na hiyo ndiyo njia ambayo yapasa kutukia, acheni afanye lile atakalo; hafanyi dhambi. Acheni waoe au waolewe.” (1 Wakorintho 7:36, NW) Lile neno moja la Kigiriki (hy·peʹra·kmos) ambalo limetafsiriwa “umepita mchanuko wa ujana” lamaanisha kihalisi “kupita kilele cha juu zaidi” na hurejezea kupita kilele cha msukumo wa tamaa ya kingono. Kwa hiyo wale ambao wamekuwa katika hali ya useja kwa miaka kadhaa na wanaohisi hatimaye kwamba wapaswa kufunga ndoa wako huru kabisa kufunga ndoa na mwamini mwenzao.—2 Wakorintho 6:14.
-
-
Mume na Mzee—Kusawazisha Hayo MadarakaMnara wa Mlinzi—1996 | Oktoba 15
-
-
1, 2. Kwa nini useja wa mapadri si wa Kimaandiko?
KATIKA karne ya kwanza, Wakristo waaminifu walihangaikia kusawazisha madaraka yao mbalimbali. Mtume Paulo aliposema kwamba Mkristo anayedumu akiwa mseja “atazidi kufanya vema,” je, alimaanisha kwamba mwanamume huyo angefaa zaidi kutumikia akiwa mwangalizi katika kutaniko la Kikristo? Je, alikuwa akifanya useja kuwa takwa la kuwa mzee? (1 Wakorintho 7:38) Useja ni takwa kwa makasisi Wakatoliki. Lakini je, useja wa mapadri ni wa Kimaandiko? Makanisa ya Othodoksi ya Mashariki huruhusu mapadri wao wa parokia wawe wanaume waliooa, lakini hawaruhusu maaskofu wao wafanye hivyo. Je, hilo lapatana na Biblia?
2 Wengi wa mitume 12 wa Kristo, washiriki wa msingi wa kutaniko la Kikristo, walikuwa wanaume waliooa. (Mathayo 8:14, 15; Waefeso 2:20) Paulo aliandika hivi: “Je, hatuna ruhusa kumchukua mke Mkristo katika ziara zetu, kama vile wafanyavyo mitume wengine, ndugu zake Bwana, na pia Kefa [Petro]?” (1 Wakorintho 9:5, Habari Njema kwa Watu Wote) Kichapo New Catholic Encyclopedia chakubali kwamba “chanzo cha sheria ya useja ni cha kikanisa” na kwamba “wahudumu katika AJ [Agano Jipya] hawakuwa chini ya wajibu wa useja.” Mashahidi wa Yehova hufuata kigezo cha Kimaandiko badala ya sheria ya kikanisa.—1 Timotheo 4:1-3.
Kuwa Mzee na Ndoa Ni Mambo Yanayopatana
3. Ni mambo gani ya hakika ya Kimaandiko yaonyeshayo kwamba waangalizi Wakristo waweza kuwa wanaume waliooa?
3 Badala ya kutaka kwamba wanaume waliowekwa rasmi wawe waangalizi wasioe, Paulo alimwandikia Tito hivi: “Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee [Kigiriki, pre·sbyʹte·ros] katika kila mji kama vile nilivyokuamuru; ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii. Maana imempasa askofu [“mwangalizi,” NW] [Kigiriki, e·piʹsko·pos, litokapo neno “askofu”] awe mtu asiyeshitakiwa neno, kwa kuwa ni wakili wa Mungu.”—Tito 1:5-7.
-