-
Dhuluma Tatizo la Ulimwenguni PoteAmkeni!—2003 | Agosti 22
-
-
Dhuluma Tatizo la Ulimwenguni Pote
“Ukija shuleni kesho, tutakuua.” —Mwanafunzi anayeitwa Kristen huko Kanada alipokea tisho hilo alipopigiwa simu na msichana ambaye hakutaja jina lake.a
“Kwa kawaida siathiriwi sana kihisia, lakini mambo yalizidi kiasi cha kwamba sikutaka kwenda shuleni. Niliumwa na tumbo, na kila asubuhi baada ya kula nilitapika.”—Hiromi, mwanafunzi huko Japan, anaeleza jinsi alivyodhulumiwa.
-
-
Dhuluma Tatizo la Ulimwenguni PoteAmkeni!—2003 | Agosti 22
-
-
Kristen, msichana aliyetajwa mwanzoni, alidhulumiwa na wanafunzi wenzake kwa miaka mingi. Alipokuwa katika shule ya msingi, wanafunzi waliomdhulumu walikuwa wakitia chingamu kwenye nywele zake, walikuwa wakimfanyia mzaha kuhusu sura yake, na kumtisha kwamba wangempiga. Alipokuwa katika shule ya sekondari, mambo yalizidi kiasi cha kwamba alipokea vitisho kupitia simu. Sasa akiwa na umri wa miaka 18, anasema hivi kwa masikitiko: “Mtu huenda shuleni kusoma, bali si kuteswa au kutishwa kwamba atauawa.”
-
-
Dhuluma Tatizo la Ulimwenguni PoteAmkeni!—2003 | Agosti 22
-
-
Dhuluma Iko Ulimwenguni Kote
Ulimwenguni kote watoto wenye umri wa kwenda shule hukabili dhuluma. Uchunguzi uliofanywa na kuchapishwa katika gazeti la Pediatrics in Review ulionyesha kwamba asilimia 14 ya watoto huko Norway huwadhulumu wengine au hudhulumiwa. Nchini Japan, asilimia 15 ya wanafunzi wa shule za msingi wanasema kwamba wao hudhulumiwa, na asilimia 17 hudhulumiwa huko Australia na Hispania. Mtaalamu mmoja anakadiria kwamba watoto milioni 1.3 hudhulumiwa au kuwadhulumu wengine nchini Uingereza.
Profesa Amos Rolider wa Chuo cha Emek Yizre’el aliwahoji wanafunzi 2,972 wa shule 21. Kulingana na gazeti The Jerusalem Post, profesa huyo aligundua kuwa “asilimia 65 walilalamika kwamba walipigwa makofi au mateke, walisukumwa, na kunyanyaswa na wanafunzi wenzao.”
-