Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • UKIMWI Utakwisha Lini?
    Amkeni!—2004 | Novemba 22
    • UKIMWI Utakwisha Lini?

      Tangu wakiwa wachanga, vijana huathiriwa na habari nyingi kuhusu ngono ambazo huwashawishi kuishi maisha mapotovu. Watu wengi hujidunga sindano za dawa za kulevya ambazo pia hueneza sana virusi vya UKIMWI. Kwa kuwa kuna upotovu mwingi ulimwenguni na maoni ya kutojali, huenda ukajiuliza ikiwa UKIMWI utakwisha.

      KWA kufaa, wataalamu wa afya wanasema kwamba mabadiliko katika tabia za watu ni njia muhimu ya kupambana na UKIMWI. Ripoti moja iliyochapishwa na Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa ilisema kwamba “kila kizazi cha vijana kinahitaji kuendelea kuelimishwa sana kuhusu afya na kusaidiwa kujua jinsi ya kuepuka tabia zinazoweza kusababisha waambukizwe virusi vya UKIMWI. Wazazi na walimu wanapaswa kuhusishwa katika miradi hiyo ya kuwaelimisha vijana.”

      Kwa wazi, wazazi wanahitaji kuwaelimisha watoto wao kuhusu hatari hizo kabla hawajapotoshwa na marafiki zao. Hilo si jambo rahisi, lakini linaweza kuokoa uhai wa mtoto wako. Huwezi kuwaharibu watoto wako kwa kuwafahamisha kuhusu ngono na matumizi ya dawa za kulevya. Kuwafahamisha mambo hayo kunaweza kuwazuia wasiharibike.

      Ni Muhimu Wazazi Wawazoeze Watoto Wao

      Wazazi waliomwabudu Mungu nyakati za kale walipaswa kuwafundisha watoto wao kuhusu ngono na jinsi wanavyoweza kutunza afya yao. Kwa kupendeza, sheria ambazo Waisraeli wa kale walipewa zilitia ndani miongozo hususa ya kiadili na vilevile mazoea ambayo walipaswa kuepuka ili wasipatwe na maambukizo. (Mambo ya Walawi 18:22, 23; 19:29; Kumbukumbu la Torati 23:12, 13) Watu wangefundishwaje sheria hizo? Yehova Mungu aliwaambia Waisraeli hivi: “Maneno haya ninayokuamuru leo lazima yawe moyoni mwako.” Kwanza, wazazi walipaswa kuelewa faida za kufuata sheria hizo na madhara ya kutozifuata. Kisha wakaagizwa hivi: “Uyakazie kwa mwana wako na kuyasema unapoketi katika nyumba yako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamka.”—Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.

      Neno la Kiebrania linalotafsiriwa ‘kazia’ linamaanisha “kurudia,” “kusema tena na tena,” au “kuingiza.” Bila shaka, wakati unahitajiwa ili kufanya hivyo. Wazazi wanaotenga wakati ili kuwafundisha wana na binti zao kuhusu hatari za matumizi ya dawa za kulevya na ngono haramu, wanaweza kufurahia kuwaona watoto wao wakiepuka tabia zinazoweza kuwafanya waambukizwe virusi vya UKIMWI na magonjwa mengine.a

  • UKIMWI Utakwisha Lini?
    Amkeni!—2004 | Novemba 22
    • a Wazazi wengi wameona kwamba kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova, ni kifaa muhimu cha kuwafundisha watoto wachanga hatua kwa hatua kuhusu ngono na kanuni za msingi za maadili.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki