-
Lugha Ambayo Waiona!Amkeni!—1998 | Septemba 8
-
-
Kwa Carl, anayetoka Marekani, lugha hii ilikuwa zawadi kutoka kwa wazazi wake Viziwi.b Ingawa alizaliwa akiwa kiziwi, aliweza kubandika vibandiko kwenye vitu, kuunganisha ishara, na kufafanua mambo katika Lugha ya Ishara ya Marekani (ASL) akiwa na umri mchanga sana. Watoto wengi wachanga walio Viziwi ambao wazazi wao Viziwi huwasiliana kwa ishara, huanza kutokeza ishara yao ya kwanza wanapofikia umri wa miezi 10 hadi 12. Katika kitabu A Journey Into the Deaf-World, inasemekana kwamba “wajuzi wa lugha sasa wanatambua kwamba uwezo wa kujifunza lugha kiasili na kuipitisha kwa watoto uko ndani kabisa ya akili. Kama uwezo huo utajitokeza ukiwa lugha ya ishara au inayozungumzwa si muhimu.”
Sveta alizaliwa Urusi katika familia ya Viziwi ya baba, wanawe, na mjukuu. Pamoja na ndugu yake Kiziwi, alijifunza Lugha ya Ishara ya Urusi. Wakati alipoandikishwa kwenye shule ya matayarisho ya watoto Viziwi akiwa na umri wa miaka mitatu, alikuwa amesitawisha ustadi wa kiasili katika lugha ya ishara kwa kiwango cha hali ya juu. Sveta akiri hivi: “Watoto wengine Viziwi hawakujua lugha ya ishara na wangejifunza kutoka kwangu.” Watoto wengi Viziwi walikuwa na wazazi wawezao Kusikia ambao hawakutumia lugha ya ishara. Mara nyingi watoto wachanga zaidi walifundishwa lugha ya ishara shuleni na watoto Viziwi wenye umri mkubwa zaidi, wakiwawezesha kuwasiliana kwa urahisi.
Leo wazazi wengi zaidi wawezao Kusikia wanajifunza ishara pamoja na watoto wao. Tokeo ni kwamba, Viziwi hawa wachanga wanaweza kuwasiliana kwa matokeo kabla ya kuhudhuria shule. Katika nchi ya Kanada, ndivyo ilivyokuwa kwa Andrew, ambaye wazazi wake wanaweza kusikia. Walijifunza lugha ya ishara na kuitumia pamoja naye alipokuwa na umri mchanga, wakimwandalia msingi wa lugha ambao angeweza kutegemea kwa miaka ambayo ingefuata. Sasa familia nzima yaweza kuwasiliana katika jambo lolote katika lugha ya ishara.
-
-
Lugha Ambayo Waiona!Amkeni!—1998 | Septemba 8
-
-
Vituo vingi vya elimu kwa watoto Viziwi ulimwenguni pote vimegundua manufaa ya kutumia lugha ya ishara wakati mtoto anapokuwa na umri mchanga aanzapo kujifunza lugha. (Ona masanduku katika ukurasa wa 20 na wa 22.) Vituo hivyo vimepata kwamba Kiziwi mchanga aanzapo kufunzwa lugha ya ishara ya asili na kusitawisha msingi wa lugha, atafanikiwa kielimu na kijamii na vilevile wakati wa baadaye ajifunzapo lugha iliyoandikwa.
Tume ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi, na Utamaduni kwa Viziwi lilitaarifu hivi: “Sasa haikubaliki tena kupuuza lugha ya ishara, au kuepuka kuchukua daraka kubwa katika kuikuza katika miradi ya kielimu kwa viziwi.” Ingawa hivyo, lazima isemwe kwamba, hata wazazi wafanye uamuzi upi wa kielimu kwa ajili ya watoto wao Viziwi, daraka la wazazi katika kusaidia mtoto aisitawishe ni la maana sana.—Ona makala “Nilijifunza Lugha Nyingine Ili Kuwasiliana na Mtoto Wangu,” katika Amkeni! la Novemba 8, 1996.
Kuyaelewa Maisha ya Viziwi
Watoto Viziwi wanapokuwa watu wazima, mara nyingi wanakiri kwamba walichotaka zaidi kutoka kwa wazazi wao kilikuwa mawasiliano. Wakati mamake mzee alipokuwa akifa, Jack ambaye ni Kiziwi, alijaribu kuwasiliana naye. Mamake aling’ang’ana sana kumwambia jambo fulani lakini hakuweza kuliandika na hakujua lugha ya ishara. Kisha akazimia kwa muda mrefu na baadaye akafa. Jack alisumbuliwa sana na pindi hizo za mwisho zenye kuvunja moyo. Jambo hili lilimchochea kutoa shauri hili kwa wazazi wenye watoto Viziwi: “Ikiwa mwataka kuwasiliana kwa ufasaha na kuwa na mazungumzo yenye maana, hisia-moyo na upendo pamoja na mtoto wenu kiziwi, tumieni lugha ya ishara. . . . Nimechelewa mno. Je, umechelewa mno?”
Kwa miaka mingi watu wengi wameelewa vibaya maisha ya Viziwi. Wengine wamekuwa na maoni kwamba viziwi hawajui karibu jambo lolote kwa sababu hawasikii lolote. Wazazi fulani wamewazuia kupita kiasi watoto wao Viziwi au wakawa na hofu ya kuwaruhusu kuchangamana na watoto wawezao Kusikia. Katika tamaduni fulani Viziwi wamechukuliwa kimakosa kuwa “bubu,” ingawa kwa kawaida Viziwi hawana kasoro ya sauti. Hawawezi tu kusikia. Wengine wameiona lugha ya ishara kuwa isiyostaarabika au ya hali ya chini inapolinganishwa na lugha isemwayo. Haishangazi basi kwamba kwa sababu ya hali hiyo ya kutojua, Viziwi fulani wamehisi kuwa wameonewa na kueleweka vibaya.
Akiwa mtoto mchanga huko Marekani katika miaka ya 1930, Joseph aliandikishwa katika shule ya pekee kwa watoto Viziwi ambayo ilikataza kutumiwa kwa lugha ya ishara. Mara nyingi, yeye pamoja na wanadarasa wenzake walitiwa nidhamu kwa sababu ya kutumia ishara hata wakati walipokosa kufahamu usemi wa walimu wao. Jinsi walivyotamani kuelewa na watu kuwaelewa! Wengine hukua wakiwa na elimu kidogo sana ya msingi katika nchi ambazo elimu kwa watoto Viziwi ni chache. Kwa kielelezo, mleta-habari wa Amkeni! katika Afrika Magharibi alisema hivi: “Kwa Waafrika wengi walio Viziwi maisha ni magumu na yenye taabu. Kati ya watu wote wasiojiweza, labda Viziwi ndio wamepuuzwa zaidi na ndio hawaeleweki vizuri.”
-