-
Je, Utaokolewa Mungu Atendapo?Mnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 15
-
-
Yesu aliongeza hivi: “Kwa kweli, kama siku hizo hazingekatwa ziwe fupi, hakuna mwili ambao ungeokolewa; lakini kwa sababu ya wale wachaguliwa siku hizo zitakatwa ziwe fupi.” (Mathayo 24:22, NW) Hilo lilimaanisha nini wakati huo, nalo lamaanisha nini sasa?
10. Tumeelezaje Mathayo 24:22 wakati uliopita?
10 Wakati uliopita ilielezwa kwamba “mwili ambao ungeokolewa” ulirejezea Wayahudi waliookoka ile dhiki juu ya Yerusalemu katika 70 W.K. Wakristo walikuwa wamekimbia, kwa hiyo Mungu aliweza kuruhusu Waroma walete uharibifu wa upesi. Yaani, kwa sababu ya jambo la hakika kwamba “wachaguliwa” hawakuwa hatarini, siku za dhiki ziliweza kukatwa ziwe fupi, hilo likiruhusu sehemu fulani ya “mwili” wa Kiyahudi iokolewe. Ilihisiwa kwamba Wayahudi waliookoka walifananisha wale ambao wangeokoka dhiki kubwa inayokuja katika siku yetu.—Ufunuo 7:14.
-
-
Je, Utaokolewa Mungu Atendapo?Mnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 15
-
-
12. Ni nani waliokuwa “wachaguliwa” wa karne ya kwanza ambao Mungu alipendezwa nao?
12 Kufikia 70 W.K., Mungu hakuwaona tena Wayahudi wa kiasili kuwa watu wake wachaguliwa. Yesu alionyesha kwamba Mungu alikuwa amelikataa taifa hilo na angeruhusu jiji lalo kuu, hekalu lalo, na mfumo walo wa ibada ukome. (Mathayo 23:37–24:2) Mungu alichagua taifa jipya, Israeli la kiroho. (Matendo 15:14; Warumi 2:28, 29; Wagalatia 6:16) Lilitia ndani wanaume na wanawake waliochaguliwa kutoka katika mataifa yote na waliotiwa mafuta kwa roho takatifu. (Mathayo 22:14; Yohana 15:19; Matendo 10:1, 2, 34, 35, 44, 45) Miaka kadhaa kabla ya shambulio la Sesho Galo, Petro aliwaandikia “wachaguliwa kulingana na ujuzi wa kimbele wa Mungu aliye Baba, kwa utakaso na roho.” Hao watiwa-mafuta kwa roho walikuwa “jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu.” (1 Petro 1:1, 2; 2:9, NW) Mungu angewachukua wachaguliwa hao mbinguni watawale pamoja na Yesu.—Wakolosai 1:1, 2; 3:12; Tito 1:1; Ufunuo 17:14.
13. Huenda ikawa maneno ya Yesu kwenye Mathayo 24:22 yalikuwa na maana gani?
13 Kutambulishwa huko kwa wachaguliwa ni jambo lenye kusaidia, kwa kuwa Yesu alitabiri kwamba siku za dhiki zingekatwa ziwe fupi “kwa sababu ya wachaguliwa.” Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “kwa sababu ya” (NW) laweza pia kufasiriwa “kwa ajili ya” au “kwa . . . ajili.” (Marko 2:27; Yohana 12:30; 1 Wakorintho 8:11; 9:10, 23; 11:9; 2 Timotheo 2:10; Ufunuo 2:3) Kwa hiyo yawezekana kwamba Yesu alikuwa akisema, ‘Isipokuwa kama siku hizo zinakatwa ziwe fupi, hakuna mwili utakaookolewa; lakini kwa ajili ya wachaguliwa siku hizo zitakatwa ziwe fupi.’c (Mathayo 24:22, NW) Je, jambo fulani lilitendeka lililonufaisha au lililokuwa ‘kwa ajili ya’ Wakristo wachaguliwa walionaswa katika Yerusalemu?
14. “Mwili” uliokolewaje jeshi la Kiroma lilipokimbia Yerusalemu bila kutazamiwa katika 66 W.K.?
14 Kumbuka kwamba katika 66 W.K., Waroma walipitia bara lote, wakatwaa sehemu ya juu ya Yerusalemu, nao wakaanza kuuharibu ukuta. Yosefo aeleza hivi: “Laiti angalidumu na yale mazingiwa kwa muda mrefu zaidi yeye angaliteka hilo Jiji mara moja.” Ebu jiulize, ‘Kwa nini lile jeshi lenye nguvu la Kiroma lingeacha kampeni hiyo kwa ghafula na kukimbia “kinyume kabisa cha kufikiri kuzuri”?’ Rupert Furneaux, stadi wa kufafanua historia ya kijeshi, aeleza hivi: “Hakuna mwanahistoria ambaye amefanikiwa katika kutoa sababu yoyote ifaayo kwa ule uamuzi wa Galo wa ajabu na wenye kuleta msiba.” Lakini hata sababu iwe ni nini, tokeo lilikuwa kwamba hiyo dhiki ilikatwa iwe fupi. Warumi walikimbia, huku Wayahudi wakiwashambulia walipokuwa wakienda zao. Namna gani wale “wachaguliwa” Wakristo watiwa-mafuta waliokuwa wamenaswa? Kukomeshwa kwa mazingiwa kulimaanisha kwamba waliokolewa na machinjo yoyote yaliyotisha wakati wa hiyo dhiki. Kwa sababu hiyo, wale Wakristo walionufaika na kule kukatwa kwa dhiki ya mwaka wa 66 W.K. iwe fupi walikuwa ndio “mwili” uliookolewa unaotajwa kwenye Mathayo 24:22.
-