Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Endelea Kunifuata”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Bila shaka, anakasirishwa na dini zote zinazodai kwa uwongo kwamba zinamwakilisha. Alitabiri jambo hilo aliposema: “Si kila mtu anayeniambia, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika ufalme wa mbinguni, bali yule anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni ndiye atakayeingia. Wengi wataniambia siku hiyo, ‘Bwana, Bwana, . . . [hatu]kufanya matendo mengi yenye nguvu katika jina lako?’ Na hata hivyo nitawaambia waziwazi: Sikuwajua ninyi kamwe! Ondokeni kwangu, ninyi wenye matendo ya uasi-sheria.”—Mathayo 7:21-23.

      11-13. Kwa nini huenda wengine wakashangazwa na maneno makali ya Yesu kuelekea wale wanaofanya “matendo mengi yenye nguvu” katika jina lake, hata hivyo, kwa nini anakasirika? Toa mfano.

      11 Huenda wengi wa wale wanaojiita Wakristo leo wakashangazwa na maneno hayo. Kwa nini Yesu awashutumu vikali watu ambao wamekuwa wakifanya “matendo mengi yenye nguvu” katika jina lake? Dini zinazodai kuwa za Kikristo zimetoa misaada, zimewasaidia maskini, zimejenga hospitali na shule, na kufanya matendo mengine mengi. Ili kuelewa ni kwa nini Yesu amekasirishwa nao, fikiria mfano huu.

      12 Baba na mama wanataka kusafiri. Hawawezi kwenda pamoja na watoto wao, kwa hiyo wanamwajiri yaya. Wanampa maagizo haya rahisi: “Watunze watoto wetu. Uwalishe, uhakikishe kwamba wako safi, na kuhakikisha kwamba wako salama salimini.” Hata hivyo, wazazi wanaporudi wanashangaa kuona kwamba watoto wao wamedhoofika kwa kukosa chakula. Ni wachafu, wagonjwa, na wenye huzuni. Wanamlilia yaya, lakini anawapuuza. Kwa nini? Yuko juu kwenye ngazi, akiosha madirisha. Wakiwa wamekasirika, wazazi hao wanataka kujua ni kwa nini anawapuuza watoto hao. Yaya huyo anajibu: “Angalieni mambo yote niliyofanya! Nimeosha madirisha! Pia nimerekebisha nyumba! Nimefanya yote hayo kwa faida yenu!” Je, hilo litatuliza hasira ya wazazi hao? Hapana! Hawakumwambia afanye kazi hizo; walitaka tu awatunze watoto wao. Hasira yao inawaka kwa sababu hakutii maagizo yao.

      13 Dini zinazodai kuwa za Kikristo zimetenda kama yaya huyo. Yesu aliwapa maagizo wawakilishi wake wawalishe watu kiroho kwa kuwafundisha kweli ya Neno la Mungu na kuwasaidia wawe safi kiroho. (Yohana 21:15-17) Hata hivyo, dini hizo zimeshindwa kabisa kutii maagizo yake. Zimewaacha watu wakiwa na njaa ya kiroho, wakiwa wamechanganyikiwa na mafundisho ya uwongo, bila ufahamu wa kweli za msingi za Biblia. (Isaya 65:13; Amosi 8:11) Jitihada zake za kuboresha ulimwengu huu hazipaswi kuwa kisingizio cha kutotii kimakusudi. Isitoshe, ulimwengu huu ni kama nyumba inayokusudiwa kubomolewa! Neno la Mungu linaonyesha wazi kwamba ulimwengu wa Shetani utaharibiwa karibuni.—1 Yohana 2:15-17.

  • “Endelea Kunifuata”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • 15, 16. (a) Yesu anahisije kuhusu ukosefu wa upendo ambao umeenea sana leo, nasi tunajuaje kwamba anahisi hivyo? (b) Kwa nini dini zinazodai kuwa za Kikristo zinamkasirisha Yesu?

      15 Tuna hakika kwamba Mfalme huyo hukasirika anapoona ukosefu wa upendo ambao umeenea sana duniani leo. Huenda tunakumbuka jinsi Mafarisayo walivyomchambua Yesu kwa kuponya watu siku ya Sabato. Mafarisayo walikuwa na mioyo migumu na vichwa vigumu sana hivi kwamba walishikilia tu maoni yao yaliyopotoka kuhusu Sheria ya Musa na sheria ya mdomo. Miujiza ya Yesu ilitimiza mambo mengi mema! Hata hivyo, miujiza hiyo iliyoleta shangwe, kitulizo, na kuitia nguvu imani ya watu haikuwa na maana yoyote kwao. Yesu alihisije kuwahusu? Pindi moja, ‘aliwatazama huku na huku kwa ghadhabu, akiwa amehuzunishwa na jinsi mioyo yao ilivyokuwa migumu.’—Marko 3:5.

      16 Leo, Yesu anaona mengi zaidi ‘yanayomhuzunisha’ sana. Viongozi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo wamepofushwa kwa sababu wameazimia kufuata mapokeo na mafundisho ambayo hayapatani na Maandiko. Isitoshe, wanakasirishwa na kazi ya kuhubiriwa kwa habari njema ya Ufalme wa Mungu. Katika sehemu nyingi za ulimwengu, makasisi wamechochea mateso makali dhidi ya Wakristo wanaojitahidi kikweli kuhubiri ujumbe ambao Yesu alihubiri. (Yohana 16:2; Ufunuo 18:4, 24) Wakati huohuo, mara nyingi makasisi hao wanawahimiza wafuasi wao wenyewe waende vitani kuwaua wengine, kana kwamba kufanya hivyo kutamfurahisha Yesu Kristo!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki