Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • Ikiwa wewe ni mwanamume uliyebatizwa, unaweza kufanya nini ili ustahili kuwa mtumishi wa huduma na baadaye mzee wa kutaniko? Kadiri maelfu ya wapya wanavyoendelea kumiminika katika tengenezo la Mungu, ndivyo kunavyokuwa na uhitaji mkubwa wa ndugu wanaostahili kuongoza. Kitabu hiki kitakusaidia kuelewa mambo yanayohusika ili ‘ujitahidi’ kufikia mapendeleo hayo ya kiroho.—1 Tim. 3:1.

      Tunasali kwa dhati kwamba kitabu hiki kitakusaidia kutambua sehemu yako katika mpango wa Yehova na kuithamini. Tunawapenda sana ninyi nyote na tunaendelea kusali kwamba mtakuwa miongoni mwa wale ambao wataendelea kushangilia milele katika kumwabudu Baba yetu wa mbinguni, Yehova.—Zab. 37:10, 11; Isa. 65:21-25.

      Ndugu zenu,

      Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

  • Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • SURA YA 1

      Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova

      ULIMWENGUNI pote, kuna mashirika mengi ya kidini, kisiasa, kibiashara, na kijamii yenye mpangilio, malengo, maoni, na falsafa mbalimbali. Lakini kuna tengenezo moja lililo tofauti kabisa na mashirika mengine yote. Neno la Mungu linaonyesha waziwazi kwamba tengenezo hilo ni Mashahidi wa Yehova.

      2 Inafurahisha kwamba umeanza kushirikiana na tengenezo la Yehova. Baada ya kujihakikishia mwenyewe mapenzi ya Mungu, sasa unayafanya. (Zab. 143:10; Rom. 12:2) Wewe ni mhudumu mwenye bidii anayeshirikiana na ushirika wenye upendo wa akina ndugu ulimwenguni pote. (2 Kor. 6:4; 1 Pet. 2:17; 5:9) Kama vile Neno la Mungu linavyoahidi, kufanya hivyo kunakuletea baraka na furaha nyingi. (Met. 10:22; Marko 10:30) Kwa kufanya mapenzi ya Yehova kwa uaminifu, unatayarishwa kufurahia uzima wa milele wakati ujao.—1 Tim. 6:18, 19; 1 Yoh. 2:17.

      3 Muumba wetu Mkuu ana tengenezo la pekee la ulimwenguni pote linaloongozwa kitheokrasi. Hilo linamaanisha kwamba Yehova ndiye anayelitawala akiwa Kichwa cha wote. Tunamtumaini kabisa. Yeye ndiye Mwamuzi wetu, Mpaji-sheria wetu, na Mfalme wetu. (Isa. 33:22) Kwa kuwa yeye ni Mungu mwenye utaratibu, amefanya mipango inayotuwezesha ‘kufanya kazi pamoja naye’ ili kutimiza kusudi lake.—2 Kor. 6:1, 2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki