Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakumbukeni Wale Wanaoongoza Kati Yenu”
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • inaongoza mambo. Sehemu inayoonekana ya tengenezo la Yehova imepata baraka nyingi. Kwa hiyo, tunaiunga mkono kikamili na kuitumaini kabisa.

      JINSI TUNAVYOIUNGA MKONO

      12 Wale ambao wamepewa majukumu kutanikoni wanaonyesha kwamba wanaunga mkono wale wanaoongoza kwa kukubali na kutimiza kwa uaminifu majukumu yao. (Mdo. 20:28) Tukiwa watangazaji wa Ufalme, tunashiriki kwa bidii katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba, kufanya ziara za kurudia, na kuongoza mafunzo ya Biblia. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Ili tufaidike kikamili na chakula kingi cha kiroho kinachotayarishwa na mtumwa mwaminifu, tunajitayarisha na kuhudhuria mikutano na makusanyiko ya Kikristo. Sisi hufaidika sana kwa kutiana moyo tunaposhirikiana kwa uhuru na ndugu zetu katika mikutano na makusanyiko hayo ya Kikristo.—Ebr. 10:24, 25.

      13 Tunapotoa vitu vyetu vya kimwili ili kuunga mkono tengenezo, tunaonyesha kwamba tunalitumaini kabisa. (Met. 3:9, 10) Tunapoona kwamba ndugu zetu wana uhitaji wa kimwili, tunawasaidia bila kukawia. (Gal. 6:10; 1 Tim. 6:18) Tunafanya hivyo kwa roho ya upendo wa kindugu, tukiwa macho sikuzote ili kuonyesha kwamba tunamshukuru Yehova na tengenezo lake kwa sababu ya wema ambao ametuonyesha.—Yoh. 13:35.

      14 Njia nyingine ambayo tunaonyesha kwamba tunaunga mkono tengenezo ni kwa kukubali maamuzi yanayofanywa. Hilo linatia ndani kufuata kwa unyenyekevu mwongozo wa ndugu waliowekwa rasmi, kama vile waangalizi wa mzunguko na wazee wa makutaniko. Ndugu hao ni miongoni mwa “wale wanaoongoza” ambao tunapaswa kuwatii na kuwanyenyekea. (Ebr. 13:7, 17) Ingawa huenda tusielewe kikamili sababu ya maamuzi fulani, tunajua kwamba tukiyaunga mkono, tutapata faida za kudumu. Matokeo ni kwamba Yehova hutubariki tunapotii Neno lake na tengenezo lake. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba tunamtii Bwana wetu, Yesu Kristo.

      15 Naam, tuna sababu nyingi za kumtumaini mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Shetani, mungu wa mfumo huu wa mambo, anajitahidi juu chini kulivunjia heshima jina la Yehova na tengenezo lake. (2 Kor. 4:4) Usijiruhusu kamwe unaswe na mbinu zenye uovu za Shetani! (2 Kor. 2:11) Anajua kwamba ana “kipindi kifupi cha wakati” kabla hajatupwa ndani ya abiso, naye ameazimia kuwapotosha Wakristo wengi iwezekanavyo wamwasi Mungu. (Ufu. 12:12) Hata hivyo, kadiri Shetani anavyozidisha jitihada zake, na tuendelee kumkaribia Yehova zaidi. Acheni tuendelee kumtumaini Yehova na njia anayotumia kuwaelekeza watu wake leo. Tukifanya hivyo, tutakuwa na undugu wenye umoja.

  • Mipango na Usimamizi Katika Kutaniko
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • SURA YA 4

      Mipango na Usimamizi Katika Kutaniko

      KATIKA barua yake ya kwanza kwa Wakorintho, mtume Paulo alieleza kweli muhimu kumhusu Mungu. Aliandika hivi: “Mungu si Mungu wa machafuko, bali ni wa amani.” Kisha, akieleza zaidi kuhusu mikutano ya kutaniko, alisema hivi: “Mambo yote na yatendeke kwa adabu na kwa mpango.”—1 Kor. 14:33, 40.

      2 Mwanzoni mwa barua hiyohiyo, mtume Paulo alionya kuhusu ugomvi uliokuwa katika kutaniko la Korintho. Paulo aliwahimiza akina ndugu ‘waseme kwa upatano’ na ‘waunganishwe kabisa katika akili ileile na njia ileile ya kufikiri.’ (1 Kor. 1:10, 11) Kisha aliwashauri kuhusu mambo mbalimbali yaliyokuwa yakivuruga umoja wa kutaniko. Akitumia mfano wa mwili wa mwanadamu, alionyesha uhitaji wa kuwa na umoja na ushirikiano. Aliwahimiza washiriki wote wa kutaniko la Kikristo, haidhuru walikuwa na majukumu gani, watunzane kwa upendo. (1 Kor. 12:12-26) Ushirikiano mzuri miongoni mwa wale walio kutanikoni unadhihirisha kwamba kutaniko lingekuwa limepangwa vizuri.

      3 Hata hivyo, kutaniko la Kikristo lilipaswa kuwa na mpangilio gani? Ni nani ambaye angelipanga? Lingekuwa na muundo gani? Ni nani wangepewa majukumu? Biblia inajibu maswali hayo.—1 Kor. 4:6.

      MPANGILIO WA KITHEOKRASI

      4 Kutaniko la Kikristo lilianzishwa katika siku ya Pentekoste mwaka wa 33 W.K. Tunajifunza nini kuhusu kutaniko hilo la karne ya kwanza? Lilipangwa na kusimamiwa kitheokrasi, yaani, lilikuwa chini ya utawala wa Mungu (Kigiriki, the·osʹ na kraʹtos). Maneno hayo mawili ya Kigiriki yanapatikana kwenye 1 Petro 5:10, 11. Masimulizi ya Biblia kuhusu mambo yaliyotendeka Yerusalemu karibu miaka 2,000 iliyopitia yanathibitisha wazi kwamba kutaniko hilo la Wakristo watiwa-mafuta lilianzishwa na Mungu. (Mdo. 2:1-47) Lilikuwa jengo lake, nyumba yake. (1 Kor. 3:9; Efe. 2:19) Leo, kutaniko la Kikristo linafuata utaratibu na mpangilio ambao ulianzishwa katika karne ya kwanza.

      Leo, kutaniko la Kikristo linafuata utaratibu na mpangilio ambao ulianzishwa katika karne ya kwanza

      5 Kutaniko la mapema lilianza na wanafunzi 120 hivi. Andiko la Yoeli 2:28, 29 lilitimizwa wakati roho takatifu ilipomiminwa juu ya wanafunzi hao. (Mdo. 2:16-18) Hata hivyo siku hiyohiyo, karibu watu wengine 3,000 walibatizwa katika maji na kujiunga na kutaniko hilo la watiwa-mafuta. Walikuwa wamekubali ujumbe kumhusu Kristo nao “wakaendelea kujitoa kwa bidii kwa fundisho la mitume.” Kisha, “Yehova akaendelea kuwaongezea kila siku watu waliokuwa wakiokolewa.”—Mdo. 2:41, 42, 47.

      6 Kulikuwa na ongezeko kubwa katika kutaniko la Yerusalemu hivi kwamba kuhani mkuu wa Wayahudi

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki