-
Kudumisha Amani na Usafi wa KutanikoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
kumjulisha uamuzi huo, na kumweleza wazi sababu ya (za) Kimaandiko ya (za) kumtenga na ushirika. Inapomjulisha mkosaji uamuzi wao, halmashauri ya hukumu itamwambia kwamba ikiwa anahisi kuwa wamekosea katika uamuzi waliofanya na angependa kukata rufaa, anapaswa kufanya hivyo kupitia barua, akieleza waziwazi sababu zake za kukata rufaa. Atapewa siku saba za kufanya hivyo tangu uamuzi wa hukumu ulipotolewa. Ikiwa baraza la wazee limepokea rufaa, linapaswa kuwasiliana na mwangalizi wa mzunguko, ambaye atachagua wazee wanaostahili watumikie wakiwa halmashauri ya rufaa ili wasikilize kesi hiyo tena. Wazee hao watajitahidi kusikiliza kesi hiyo kabla juma moja halijapita baada ya kupokea barua hiyo. Ikiwa mkosaji amekata rufaa, tangazo la kutengwa na ushirika litaahirishwa. Katika kipindi hicho, mshitakiwa atazuiwa kutoa maelezo na sala kwenye mikutano na kuzuiwa mapendeleo ya pekee ya utumishi.
27 Kuruhusiwa kukata rufaa ni tendo la fadhili linalompa mshtakiwa nafasi nyingine ya malalamiko yake kusikilizwa. Hivyo, ikiwa mkosaji hajafika kimakusudi kwenye kikao cha rufaa, tangazo la kutengwa na ushirika litatangazwa baada ya wazee kujitahidi kadiri wawezavyo kuwasiliana naye.
28 Ikiwa mkosaji hangependa kukata rufaa, halmashauri ya hukumu itamweleza kuhusu uhitaji wa kutubu na vilevile hatua anazoweza kuchukua ili arudishwe baada ya muda. Kufanya hivyo ni njia ya kumsaidia na kumwonyesha fadhili, nao wazee wanapaswa kufanya hivyo wakitumaini kwamba atabadili njia zake na baadaye astahili kurudi katika tengenezo la Yehova.—2 Kor. 2:6, 7.
TANGAZO LA KUTENGA NA USHIRIKA
29 Inapokuwa lazima kumtenga na ushirika wa kutaniko mkosaji asiyetubu, tangazo fupi hutolewa linalosema: “[Jina la mtu] si mmoja wa Mashahidi wa Yehova tena.” Hilo litawatahadharisha ndugu na dada waaminifu kutanikoni waache kushirikiana na mtu huyo.—1 Kor. 5:11
KUJITENGA NA USHIRIKA
30 Usemi “kujitenga na ushirika” hurejelea hatua inayochukuliwa na mtu ambaye ni Shahidi aliyebatizwa lakini anakana kimakusudi msimamo wake wa Kikristo kwa kusema kwamba hataki tena kutambuliwa, au kujulikana kuwa Shahidi wa Yehova. Au huenda amelikana kutaniko la Kikristo kupitia matendo yake, kama vile kwa kujiunga na shirika la kilimwengu lenye malengo yanayopingana na mafundisho ya Biblia ambalo litahukumiwa na Yehova Mungu.—Isa. 2:4; Ufu. 19:17-21.
31 Mtume Yohana aliandika hivi kuhusu wale walioikana imani ya Kikristo katika siku zake: “Waliondoka miongoni mwetu, lakini hawakuwa wa namna yetu; kwa maana kama wangekuwa wa namna yetu, wangebaki pamoja nasi.”—1 Yoh. 2:19.
32 Machoni pa Yehova, hali ya mtu aliyejitenga na ushirika ni tofauti kabisa na ya Mkristo asiyetenda ambaye hashiriki tena katika huduma ya shambani. Huenda mtu asiyetenda aliacha kujifunza Neno la Mungu kwa ukawaida. Au labda amepoteza bidii yake ya kumtumikia Yehova kwa sababu ya matatizo ya kibinafsi au mateso. Wazee na wengine kutanikoni wataendelea kumpa Mkristo huyo asiyetenda msaada wa kiroho unaofaa.—Rom. 15:1; 1 The. 5:14; Ebr. 12:12.
33 Hata hivyo, kwa Mkristo ambaye ameamua mwenyewe kujitenga na ushirika, tangazo hili fupi litatolewa ili kulijulisha kutaniko: “[Jina la mtu] si mmoja wa Mashahidi wa Yehova tena.” Mtu huyo hutendewa sawa na mtu aliyetengwa na ushirika.
KURUDISHWA
34 Mtu aliyetengwa na ushirika au yule aliyejitenga na ushirika wa kutaniko anaweza kurudishwa akionyesha wazi kwamba ametubu na muda wa kutosha umepita ili kuonyesha kwamba ameacha mwenendo wake wenye dhambi. Anaonyesha kwamba anatamani kuwa na uhusiano mzuri na Yehova. Wazee huwa waangalifu kwa kuruhusu muda wa kutosha upite—miezi mingi, mwaka, au muda mrefu zaidi, ikitegemea hali—ili mtu huyo athibitishe kwamba ametubu kikweli. Baraza la wazee linapopokea barua ya ombi la kutaka kurudishwa, halmashauri ya kurudisha itazungumza na mtu huyo. Halmashauri hiyo itachunguza uthibitisho wa “matendo yanayoonyesha toba” kwa mkosaji huyo na kuamua ikiwa itamrudisha wakati huo au la.—Mdo. 26:20.
35 Ikiwa mtu anayeomba kurudishwa alitengwa na kutaniko lingine, halmashauri ya kurudisha ya kutaniko la mahali alipo itakutana naye na kufikiria ombi lake. Ikiwa washiriki wa halmashauri hiyo wanaamini kwamba mtu huyo anapaswa kurudishwa, watatuma pendekezo lao kwenye baraza la wazee la kutaniko ambalo lilishughulikia kisa hicho. Halmashauri zinazohusika zitashirikiana ili kuhakikisha mambo yote yamechunguzwa na uamuzi unaofaa umefanywa. Hata hivyo, uamuzi wa kumrudisha utafanywa na halmashauri ya kurudisha ya kutaniko lililoshughulikia kisa hicho.
TANGAZO LA KURUDISHWA
36 Halmashauri ya kurudisha ikisadikishwa kwamba mtu aliyetengwa na ushirika au aliyejitenga na ushirika ametubu kikweli na anastahili kurudishwa, tangazo la kumrudisha hutolewa katika kutaniko lililoshughulikia kisa chake. Ikiwa sasa mtu huyo yuko kutaniko lingine, tangazo litatolewa katika kutaniko hilo pia. Tangazo hilo linapaswa kusema: “[Jina la mtu] amerudishwa, naye sasa ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova.”
VISA VINAVYOHUSU WATOTO AMBAO WAMEBATIZWA
37 Makosa mazito yanayofanywa na watoto ambao wamebatizwa yanapaswa kuripotiwa kwa wazee. Wazee wanaposhughulikia makosa mazito yanayowahusu watoto, inafaa wazazi waliobatizwa wa mtoto huyo wawepo. Itafaa washirikiane na halmashauri ya hukumu, bali si kujaribu kumtetea mtoto aliyefanya kosa ili asichukuliwe hatua ya kutiwa nidhamu. Sawa na vile inavyoshughulikia watu wazima waliofanya kosa, halmashauri ya hukumu hujitahidi kumkaripia na kumrekebisha mkosaji. Hata hivyo, ikiwa mtoto huyo haonyeshi toba, hatua ya kumtenga na ushirika itachukuliwa.
WAHUBIRI AMBAO HAWAJABATIZWA WANAPOFANYA KOSA
38 Namna gani ikiwa wahubiri ambao hawajabatizwa wamefanya makosa mazito? Kwa kuwa wao si Mashahidi waliobatizwa, hawawezi kutengwa na ushirika. Hata hivyo, labda hawaelewi vizuri viwango vya Biblia, na huenda wakahitaji kushauriwa kwa busara ili kuwasaidia waifanyie miguu yao “mapito yaliyonyooka.”—Ebr. 12:13.
39 Ikiwa mhubiri ambaye hajabatizwa hajaonyesha toba baada ya wazee wawili kukutana naye na kujaribu kumsaidia, basi kutaniko linahitaji kujulishwa. Tangazo fupi hutolewa linalosema: “[Jina la mtu] hatambuliwi tena kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa.” Kisha, kutaniko litamwona mkosaji huyo kama mtu wa ulimwengu. Ingawa mkosaji huyo hatengwi na ushirika, Wakristo huwa waangalifu wanaposhirikiana naye. (1 Kor. 15:33) Hatakubaliwa kutoa ripoti za utumishi wa shambani.
40 Baada ya muda, huenda mhubiri ambaye hajabatizwa aliyeondolewa kuwa mhubiri, akataka tena kuwa mhubiri. Katika hali hiyo, wazee wawili watakutana naye ili kuchunguza maendeleo yake ya kiroho. Ikiwa anastahili, tangazo fupi linaweza kutolewa linalosema: “[Jina la mtu] anatambuliwa tena kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa.”
YEHOVA HUBARIKI IBADA SAFI NA YENYE AMANI
41 Wote wanaoshirikiana na kutaniko la Mungu leo wanaweza kufurahia paradiso ya kiroho ambayo Yehova amewapa watu wake. Tuna chakula kingi cha kiroho na maji mengi yenye kuburudisha ya kweli. Pia, tunalindwa na Yehova kupitia mpango wake wa kitheokrasi chini ya ukichwa wa Kristo. (Zab. 23; Isa. 32:1, 2) Kuwa katika paradiso ya kiroho katika siku hizi zenye taabu kumetufanya tujihisi tukiwa salama.
Tunapodumisha amani na usafi wa kutaniko, tunaendelea kuacha nuru yetu ya kweli ya Ufalme iangaze
42 Tunapodumisha amani na usafi wa kutaniko, tunaendelea kuacha nuru yetu ya kweli ya Ufalme iangaze. (Mt. 5:16; Yak. 3:18) Mungu atatubariki, nasi tutashangilia kuona watu wengi zaidi wakimjua Yehova na wakijiunga nasi ili kufanya mapenzi yake.
-
-
Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa KitheokrasiTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 15
Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa Kitheokrasi
NI LAZIMA tujitiishe kwa Mungu, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote, ili tuwe sehemu ya tengenezo linalofanya mapenzi ya Yehova. Tunatambua kwamba Mwana wake ndiye Kichwa cha kutaniko la Kikristo na pia tunafuata kanuni ya ukichwa katika mambo mengine maishani. Kila mtu anayejitiisha katika mpango huo wa kitheokrasi hufaidika.
2 Wanadamu walijulishwa kwa mara ya kwanza kabisa kuhusu mpango wa kujitiisha chini ya mamlaka katika bustani ya Edeni. Mpango huo unafafanuliwa katika amri za Mungu zilizo kwenye Mwanzo 1:28 na 2:16, 17. Wanyama wangeongozwa na wanadamu, na Adamu na Hawa walipaswa kujitiisha kwa mapenzi na mamlaka ya Mungu. Kutii mamlaka ya Mungu kungeleta amani na utaratibu mzuri. Kanuni ya ukichwa inakaziwa tena katika 1 Wakorintho 11:3. Mtume Paulo aliandika hivi: “Nataka mjue kwamba kichwa cha kila mwanamume ni Kristo; nacho kichwa cha mwanamke ni mwanamume; nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.” Hilo linaonyesha kwamba kila mtu yuko chini ya ukichwa fulani katika mpango huo, isipokuwa Yehova.
3 Watu wengi leo hawaheshimu wala kutii kanuni ya ukichwa. Kwa nini? Tatizo lilianzia Edeni wazazi wa wanadamu walipochagua kimakusudi kutojitiisha chini ya ukichwa wa Mungu mwenye enzi kuu. (Mwa. 3:4, 5) Hata hivyo, hawakupata uhuru zaidi. Badala yake, walijitiisha chini ya kiumbe mwovu wa roho, Shetani Ibilisi. Uasi wa kwanza uliwatenganisha wanadamu na Mungu. (Kol. 1:21) Ndiyo sababu wanadamu wengi leo wako chini ya nguvu za yule mwovu.—1 Yoh. 5:19.
4 Tunapojifunza na kuishi kupatana na kweli ya Neno la Mungu, tunakataa kuongozwa na uvutano wa Shetani. Tukiwa Mashahidi waliojiweka wakfu na kubatizwa, tunamkubali Yehova kuwa Mtawala Mkuu wa maisha yetu. Tunakubaliana na Mfalme Daudi, aliyekiri kwamba Yehova ndiye “mkuu juu ya vyote.” (1 Nya. 29:11) Bila shaka tunakiri hivi kwa unyenyekevu: “Jueni kwamba Yehova ni Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, na sisi ni mali yake. Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.” (Zab. 100:3) Tunatambua kwamba Yehova ni mkuu na tunapaswa kujitiisha kwake kikamili kwa kuwa aliumba vitu vyote. (Ufu. 4:11) Tukiwa wahudumu wa Mungu wa kweli, tunamfuata Yesu Kristo, ambaye aliweka kielelezo kikamilifu cha kujitiisha kwa Mungu.
5 Yesu alijifunza nini kutokana na mateso yaliyompata alipokuwa duniani? Andiko la Waebrania 5:8 linajibu hivi: “Ingawa alikuwa mwana, alijifunza kutii kutokana na mateso yaliyompata.” Naam, Yesu aliendelea kujitiisha kwa ushikamanifu kwa Baba yake wa mbinguni hata alipokabili magumu. Zaidi ya hayo, Yesu hakufanya lolote kwa uamuzi wake mwenyewe. Hakusema mambo aliyotunga yeye mwenyewe; wala hakutafuta utukufu wake mwenyewe. (Yoh. 5:19, 30; 6:38; 7:16-18) Wakati wa huduma yake, alifurahia kufanya mapenzi ya Baba yake, hata ingawa alipingwa na kuteswa
-