-
Mashahidi wa Kikristo wa Yehova Katika Karne ya KwanzaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Watambulishwa na Mwenendo Mtakatifu na Upendo
Ushuhuda wa mashahidi wa karne ya kwanza wa Yehova haukuwa wa “tunda la midomo” tu. (Ebr. 13:15) Uanafunzi uliongoza maisha yote ya shahidi wa Kikristo. Kwa hiyo, si kwamba tu Wakristo hao walipiga mbiu ya imani zao, bali imani zao ziligeuza maisha zao pia. Waliondolea mbali utu wa zamani pamoja na mazoea yao yenye dhambi na kujitahidi kujivika utu mpya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu. (Kol. 3:5-10) Walikuwa wasema-kweli na wafuataji-haki, na vilevile wenye bidii na wenye kutegemeka. (Efe. 4:25, 28) Walikuwa safi kiadili—ukosefu wa adili katika ngono ulikatazwa katakata. Ndivyo na ulevi na ibada ya sanamu. (Gal. 5:19-21) Basi, ni kwa sababu nzuri kwamba Ukristo ulikuja kujulikana kuwa “Ile Njia,” njia au namna ya maisha yaliyotegemea hasa imani katika Yesu, kufuata kwa ukaribu hatua zake.—Mdo. 9:1, 2; 1 Pet. 2:21, 22, NW.
-
-
Mashahidi wa Kikristo wa Yehova Katika Karne ya KwanzaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 30]
‘Ushindi Wenye Shangwe wa Ukristo’
Vyanzo visivyo vya Kibiblia huthibitisha kwamba mwenendo mzuri na upendo ulikuwa sifa ya Wakristo wa mapema. Mwanahistoria John Lord alitaarifu hivi: “Ushindi wa kweli wenye shangwe wa Ukristo ulionekana katika kufanya wale waliodai kufuata mafundisho yao wawe watu wema. . . . Tuna ushuhuda wa kwamba wao walikuwa na maisha zisizo na lawama, walikuwa na maadili yasiyoweza kusutwa, walikuwa raia wema, na walikuwa na adabu zenye wema wa Kikristo.”—“The Old Roman World.”
-