-
‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
14. Kwa nini tunapaswa kujifunza kuwasamehe wengine, nasi tunaweza kuonyesha jinsi gani kwamba tuko tayari kusamehe?
14 Tukiwa wanafunzi wa Kristo, tunahitaji kujifunza kuwasamehe wengine. Kwa nini? Tofauti na Yesu, sisi si wakamilifu, na ndivyo na wale ambao huenda wakatukosea. Mara kwa mara, sisi sote tunajikwaa katika neno na tendo. (Waroma 3:23; Yakobo 3:2) Kwa kuwasamehe wengine ikiwa kuna msingi wa kuwaonyesha rehema, tunafungua njia ili Mungu atusamehe. (Marko 11:25) Basi, tunaweza kuonyesha jinsi gani kwamba tuko tayari kuwasamehe wale ambao huenda wakatukosea? Mara nyingi, upendo unatusaidia kuachilia makosa madogo-madogo tunayotendewa na wengine. (1 Petro 4:8) Wale waliotukosea wanapotubu kikweli, kama Petro alivyofanya, bila shaka, tungependa kumwiga Yesu kwa kuwa tayari kuwasamehe. Badala ya kuwawekea kinyongo, tunatenda kwa hekima tunapowasamehe. (Waefeso 4:32) Kwa kufanya hivyo, tunachangia amani kutanikoni, na pia amani yetu wenyewe ya akilini na moyoni.—1 Petro 3:11.
-
-
‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
18-20. (a) Tunaweza kuonyesha jinsi gani kwamba tunawatumaini waamini wenzetu? (b) Ni kwa njia gani tunaweza kuiga mfano wa Yesu wa kuwa tayari kuwapa wengine migawo? (c) Ni nini kitakachozungumziwa katika sura inayofuata?
18 Tunaweza kumwiga Yesu jinsi gani tunaposhughulika na watu wengine? Kuwatumaini waamini wenzetu kunaonyesha kwamba tunawapenda. Tusisahau kwamba upendo huangalia mambo mazuri bali si mabaya. Wakati ambapo watu wengine wanatuvunja moyo, jambo ambalo mara kwa mara linatokea, upendo utatuzuia tusikate kauli mara moja kwamba nia zao ni mbovu. (Mathayo 7:1, 2) Tukiwa na maoni yanayofaa kuhusu waamini wenzetu, tutawatendea kwa njia zenye kuwajenga badala ya kuwabomoa.—1 Wathesalonike 5:11.
19 Je, tunaweza kumwiga Yesu kwa kuwa tayari kuwapa wengine mapendeleo? Ndugu walio na madaraka kutanikoni wanapaswa kuwapa wengine migawo inayowafaa na inayotimiza kusudi fulani wakiamini kwamba ndugu hao watafanya yote wanayoweza. Kwa njia hiyo, wazee wenye uzoefu wanaweza kuwazoeza vijana wanaostahili ambao ‘wanajitahidi kufikia’ mapendeleo ya kulisaidia kutaniko. (1 Timotheo 3:1; 2 Timotheo 2:2) Mazoezi hayo ni ya maana. Yehova anapoendelea kuharakisha ukuzi wa Ufalme, wanaume wanaostahili watahitaji kuzoezwa kushughulikia ongezeko hilo.—Isaya 60:22.
-