Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Umati Mkubwa Ukamkaribia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Je, Watu Wanajisikia Huru Kukukaribia?

      19. Ni kwa njia gani tunaweza kujua ikiwa kwa kweli wengine wanajisikia huru kutukaribia?

      19 Kwa kawaida, watu hufikiri kwamba wengine wanajisikia huru kuwakaribia. Kwa mfano, watu fulani wenye mamlaka wanapenda kusema kwamba wanaweza kufikiwa kwa urahisi, na kwamba watu walio chini yao wako huru kuwafikia wakati wowote. Hata hivyo, Biblia inatoa onyo hili kali: “Wanadamu wengi hutangaza fadhili zao wenyewe zenye upendo, lakini ni nani anayeweza kumpata mtu mwaminifu?” (Methali 20:6) Ni rahisi kusema kwamba watu wanajisikia huru kutukaribia, lakini, je, sisi ni waaminifu kikweli katika kuiga upendo wa Yesu kwa njia hiyo? Jibu la swali hilo linategemea maoni ya wengine bali si yetu. Paulo alisema: “Usawaziko wenu na ujulikane kwa watu wote.” (Wafilipi 4:5) Inafaa kila mmoja wetu ajiulize: ‘Wengine wana maoni gani kunihusu? Ninajulikana kuwa mtu wa aina gani?’

      Picha katika ukurasa wa 148

      Wazee hujitahidi kuwafanya wengine wajisikie huru kuwakaribia

      20. (a) Kwa nini wazee Wakristo wanapaswa kuwafanya wengine wajisikie huru kuwakaribia? (b) Kwa nini tunapaswa kuwa wenye usawaziko kuhusiana na yale tunayotarajia kutoka kwa wazee kutanikoni?

      20 Wazee Wakristo hasa hujitahidi kuwafanya wengine wajisikie huru kuwakaribia. Wanatamani sana kutimiza yale yanayosemwa kwenye Isaya 32:1, 2: “Kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujificha kutokana na upepo na mahali pa kujificha kutokana na dhoruba ya mvua, kama vijito vya maji katika nchi isiyo na maji, kama kivuli cha mwamba mzito katika nchi iliyochoka.” Mzee anaweza kutoa ulinzi, burudisho, na kitulizo ikiwa tu ataendelea kuwafanya wengine wajisikie huru kumkaribia. Ni kweli kwamba kufanya hivyo si rahisi sikuzote kwa maana wazee wana madaraka mazito katika nyakati hizi ngumu. Lakini, wazee hujitahidi wasionekane kuwa wenye shughuli nyingi mno wasiweze kushughulikia mahitaji ya kondoo wa Yehova. (1 Petro 5:2) Washiriki wengine wa kutaniko wanajaribu kuwa wenye usawaziko kuhusiana na yale ambayo wanatarajia kutoka kwa wanaume hao waaminifu kwa kuonyesha roho ya unyenyekevu na ya ushirikiano.—Waebrania 13:17.

      21. Wazazi wanaweza kufanya nini ili watoto wajisikie huru kuwakaribia, nasi tutazungumzia nini katika sura inayofuata?

      21 Nyakati zote wazazi hujitahidi kushughulikia mahitaji ya watoto wao. Hilo ni jambo zito! Wanataka watoto wao wajue kwamba wanapaswa kujisikia huru kumweleza Baba au Mama mahangaiko yao. Hivyo, wazazi Wakristo wanajaribu kuwa wapole na wenye kukubali sababu badala ya kukasirika wakati mtoto anapoungama kosa au anapokuwa na maoni yasiyofaa. Wazazi wanapoendelea kuwazoeza watoto wao kwa subira, wao hujitahidi kuwa na mawasiliano mazuri. Kwa kweli, sote tunataka kuendelea kuwafanya wengine wajisikie huru kutukaribia, kama Yesu alivyofanya. Katika sura inayofuata, tutazungumzia jinsi Yesu alivyoonyesha huruma kutoka moyoni, mojawapo ya sifa kuu zilizofanya wengine wajisikie huru kumkaribia.

  • “Umati Mkubwa Ukamkaribia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Unaweza Kumfuata Yesu Jinsi Gani?

      • Kwa nini kuuliza maswali na kusikiliza kwa makini majibu kutawafanya wengine wajisikie huru kutukaribia?—Mathayo 16:13-17.

      • Ni kwa njia gani Yesu alifanya watu wajisikie huru kumkaribia hata wakati ambapo waliingilia wakati wake wa faragha, nasi tunaweza kufuata mfano wake jinsi gani?—Marko 6:31-34.

      • Yesu alikuwa na maoni gani kuhusu watu ambao hawakumwamini, na kuiga maoni yake yenye usawaziko kutatusaidia kwa njia gani kuwafanya wengine wajisikie huru kutukaribia?—Luka 5:29-32.

      • Ni kwa njia gani kuiga maoni ya Yesu yanayofaa kuwahusu watu kutafanya wengine wajisikie huru zaidi kutukaribia?—Yohana 1:47.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki