Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu”
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • moja, ubatizo mmoja; Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya wote, na kupitia wote na katika wote.” (Efe. 4:4-6) Maneno hayo yanatuchochea tuwe na ufahamu uleule wa mafundisho ya msingi na pia mafundisho yenye kina ya Biblia ili tuonyeshe kwamba tunatambua mamlaka kuu ya Yehova. Kwa kweli, Yehova amewapa watu wake lugha safi ya kweli inayowawezesha wamtumikie bega kwa bega.—Sef. 3:9.

      30 Umoja na amani ya kutaniko la Kikristo huwaburudisha wote wanaomwabudu Yehova. Tumeshuhudia utimizo wa ahadi hii ya Yehova: “Kwa umoja nitawaweka kama kondoo zizini.” (Mika 2:12) Tunataka kudumisha umoja na amani hiyo kwa kuishi kupatana na viwango vya uadilifu vya Yehova.

      31 Wenye furaha ni wale waliokubaliwa katika kutaniko safi la Yehova! Tunapaswa kujidhabihu kwa njia yoyote ile ili tuitwe kwa jina la Yehova. Tunapodumisha uhusiano wetu wenye thamani na Yehova, tutajitahidi sana kufuata viwango vyake vya uadilifu na kuwafundisha wengine kufanya hivyo.—2 Kor. 3:18.

  • Kudumisha Amani na Usafi wa Kutaniko
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • SURA YA 14

      Kudumisha Amani na Usafi wa Kutaniko

      KAMA unabii wa Biblia ulivyotabiri, kila mwaka maelfu ya watu humiminika kwenye nyumba ya Yehova ya ibada safi. (Mika 4:1, 2) Tunafurahia kwelikweli kuwakaribisha katika “kutaniko la Mungu”! (Mdo. 20:28) Wanathamini sana kumtumikia Yehova pamoja nasi na kufurahia mazingira safi na yenye amani ya paradiso yetu ya kiroho. Roho takatifu ya Mungu na hekima ya Neno lake inatusaidia kudumisha amani na usafi wa kutaniko.—Zab. 119:105; Zek. 4:6.

      2 Tunapofuata kanuni za Biblia, tunavaa “utu mpya.” (Kol. 3:10) Hatutilii maanani mabishano madogo-madogo na tofauti za kibinafsi. Tunashinda ushawishi unaosababisha migawanyiko ulimwenguni, na kufanya kazi kwa umoja tukiwa undugu wa kimataifa kwa sababu tuna maoni kama ya Yehova.—Mdo. 10:34, 35.

      3 Hata hivyo, mara kwa mara matatizo hutokea ambayo huathiri amani na umoja wa kutaniko. Yanasababishwa na nini? Katika visa vingi, husababishwa na kutofuata ushauri wa Biblia. Bado tunapambana na mwelekeo wetu mbaya tukiwa wanadamu wasio wakamilifu. Hakuna hata mmoja wetu asiyetenda dhambi. (1 Yoh. 1:10) Huenda mtu fulani akachukua hatua isiyofaa ambayo inaweza kuchafua maadili au usafi wa kiroho wa kutaniko. Tunaweza kumkosea mtu fulani kwa

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki