Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Magumu ya Kujua Maana ya Jina la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Julai 1
    • Baada ya Yesu kufa na kufufuliwa, wafuasi wake waaminifu waliendelea kulijulisha jina la Mungu. (Ona sanduku lenye kichwa “Je, Wakristo wa Karne ya Kwanza Walitumia Jina la Mungu?”) Katika Pentekoste 33 W.K., siku ambayo kutaniko la Kikristo lilianzishwa, mtume Petro akinukuu unabii wa Yoeli aliwaambia hivi Wayahudi na wageuzwa-imani: “Kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.” (Matendo 2:21; Yoeli 2:32) Wakristo wa mapema waliwasaidia watu kutoka mataifa mengi wajue maana ya jina la Yehova. Hivyo, mitume na wanaume wazee walipokutana Yerusalemu, mwanafunzi Yakobo alisema: ‘Mungu alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.’—Matendo 15:14.

  • Magumu ya Kujua Maana ya Jina la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Julai 1
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 6]

      Je, Wakristo wa Karne ya Kwanza Walitumia Jina la Mungu?

      Katika siku za mitume wa Yesu, makutaniko ya Kikristo yalianzishwa katika nchi nyingi. Washiriki wa makutaniko hayo walikutana kwa ukawaida ili kujifunza Biblia. Je, Wakristo hao wa karne ya kwanza walipata jina Yehova katika Biblia zao?

      Kwa kuwa Kigiriki ndiyo lugha iliyokuwa ikizungumzwa ulimwenguni pote, makutaniko mengi yalitumia tafsiri ya Maandiko ya Kiebrania iliyoitwa Septuajinti ya Kigiriki iliyokamilishwa katika karne ya pili K.W.K. Wasomi fulani wanadai kwamba tangu ilipotafsiriwa kwa mara ya kwanza, Septuajinti ilibadili jina la Mungu na kuweka jina la cheo Kyʹri·os, neno la Kigiriki linalomaanisha “Bwana.” Lakini kuna uthibitisho unaopinga madai hayo.

      Vipande vinavyoonyeshwa hapa ni sehemu ya Septuajinti ya Kigiriki iliyoandikwa karne ya kwanza K.W.K. Vipande hivyo vinaonyesha waziwazi jina la Yehova, kama linavyoandikwa katika maandishi ya Kigiriki kwa zile herufi nne za Kiebrania יהוה (YHWH), au Tetragramatoni. Profesa George Howard aliandika hivi: “Tuna nakala tatu tofauti za Biblia ya Septuajinti ya Kigiriki zilizoandikwa kabla ya Ukristo na hakuna mahali popote ambapo Tetragramatoni ilitafsiriwa kyrios au haikutafsiriwa kabisa. Sasa tunaweza kusema kwamba Wayahudi waliandika jina la Mungu . . . moja kwa moja katika Maandiko ya Kigiriki kabla ya, wakati wa, na baada ya kipindi kinachotajwa katika Agano Jipya.”—Biblical Archaeology Review.

      Je, mitume na wanafunzi wa Yesu walitumia jina la Mungu katika maandishi yao yaliyoongozwa na roho? Profesa Howard anasema hivi: “Kwa kuwa kanisa linalofafanuliwa katika Agano Jipya lilitumia na kunukuu kutoka kwenye Septuajinti iliyokuwa na jina la Mungu katika Kiebrania, hakuna shaka kwamba waandikaji wa Agano Jipya walitia ndani Tetragramatoni katika manukuu yao.”

      Kwa hiyo, tunaweza kufikia mkataa kwamba Wakristo wa karne ya kwanza wangeweza kusoma jina la Mungu katika tafsiri zao za Maandiko ya Kiebrania na pia katika nakala zao za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

      [Hisani]

      All photos: Société Royale de Papyrologie du Caire

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki