Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kusema kwa Lugha
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kusema kwa Lugha

      Maana: Uwezo wa pekee ambao wanafunzi fulani walipewa katika kutaniko la kwanza la Kikristo kupitia roho takatifu uliowawezesha kuhubiri au kumtukuza Mungu katika lugha nyingine.

      Je, Biblia inasema wote walio na roho ya Mungu ‘wangesema kwa lugha’?

      1 Kor. 12:13, 30: “Kwa kweli kwa roho moja sote tulibatizwa katika mwili mmoja . . . Je, wote wana zawadi za maponyo? Je, wote husema kwa lugha?” (Ona pia 1 Wakorintho 14:26.)

      1 Kor. 14:5: “Basi ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha, lakini napendelea zaidi kwamba mtoe unabii. Kwa kweli, yeye anayetoa unabii ni mkubwa kuliko yeye anayesema kwa lugha, isipokuwa, kwa kweli, yeye atafsiri, ili kutaniko lijengwe.”

  • Kusema kwa Lugha
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Je, ‘kusema kwa lugha’ kunakofanywa leo kunafanana na kule kwa Wakristo wa karne ya kwanza?

      Katika karne ya kwanza, zawadi za kimuujiza za roho, kutia ndani uwezo wa ‘kusema kwa lugha,’ zilithibitisha kwamba kibali cha Mungu kilikuwa kimeondolewa kutoka katika ibada ya Wayahudi na kupewa kutaniko la Kikristo lililoanzishwa karibuni. (Ebr. 2:2-4) Kwa kuwa kusudi hilo lilitimizwa katika karne ya kwanza, je, ni lazima kuthibitisha jambo hilo tena na tena katika siku zetu?

      Katika karne ya kwanza, uwezo wa ‘kusema kwa lugha’ ulisaidia kusonga mbele kwa kazi ya kutoa ushahidi kwa watu wa mataifa yote, kazi ambayo Yesu alikuwa amewaagiza wafuasi wake wafanye. (Mdo. 1:8; 2:1-11; Mt. 28:19) Je, wale ‘wanaosema kwa lugha’ wanatumia uwezo huo leo kufanya kazi hiyo?

      Katika karne ya kwanza, Wakristo ‘waliposema kwa lugha,’ mambo waliyosema yalikuwa na maana kwa watu waliojua lugha hizo. (Mdo. 2:4, 8) Leo, je, si kweli kwamba ‘kusema kwa lugha,’ mara nyingi huhusisha kupaaza sauti na kusema maneno yasiyoeleweka?

      Biblia inaonyesha kwamba katika makutaniko ya karne ya kwanza, watu wawili au watatu tu ndio walioruhusiwa ‘kusema kwa lugha’ katika mkutano mmoja; walipaswa kufanya hivyo “zamu kwa zamu,” na kama hakukuwa na mtu wa kutafsiri, walipaswa kunyamaza. (1 Kor. 14:27, 28, UV) Je, hivyo ndivyo inavyofanywa leo?

  • Kusema kwa Lugha
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Je, Wakristo wa kweli leo wanatambuliwa kwa uwezo wa ‘kusema kwa lugha’?

      Yoh. 13:35: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.”

      1 Kor. 13:1, 8: “Nikisema kwa lugha za wanadamu na za malaika lakini sina upendo, nimekuwa chombo cha shaba nyeupe kinachovuma au toazi linalolia. Upendo haushindwi kamwe. Lakini kama kuna zawadi za kutoa unabii, zitaondolewa mbali; kama kuna lugha, zitakoma.”

      Yesu alisema kwamba roho takatifu ingekuja juu ya wafuasi wake na kwamba wangekuwa mashahidi wake mpaka sehemu za mbali zaidi za dunia. (Mdo. 1:8) Aliwaagiza ‘wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ (Mt. 28:19) Pia alitabiri kwamba “hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote.” (Mt. 24:14) Ni nani leo wanaofanya kazi hiyo, wakiwa kikundi na pia watu binafsi? Kupatana na aliyosema Yesu, je, hatupaswi kutarajia jambo hilo liwe uthibitisho wa kwamba kikundi fulani kina roho takatifu?

      Je, ‘kusema kwa lugha’ kutaendelea mpaka kile kilicho “kamili” kije?

      Andiko la 1 Wakorintho 13:8 linataja zawadi kadhaa za kimuujiza—unabii, lugha, na ujuzi. Mstari wa 9 unataja vitu viwili kati ya hivyo—ujuzi na unabii—ukisema: “Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu.” (UV) Au, kama BHN inavyosema: “Maana ujuzi wetu si kamili, na kipaji chetu cha kutangaza neno la Mungu si kamili.” Kisha mstari wa 10 unasema: “Lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.” (UV) Neno “kamili” limetafsiriwa kutokana na neno la Kigiriki teʹlei·on, linalotoa wazo la kukomaa, kitu kuwa kizima, au kikamilifu. ZSB hapa imelitafsiri kuwa “kamilifu.” Ona kwamba si zawadi ya lugha inayosemwa kuwa “sehemu.” Hilo linasemwa kuhusu “unabii” na “ujuzi.” Yaani, hata wakiwa na zawadi hizo za kimuujiza, Wakristo wa kwanza walikuwa na ufahamu wa sehemu au usiokamilika wa kusudi la Mungu. Lakini wakati ambapo unabii huo ungetimizwa, wakati ambapo kusudi la Mungu lingetimizwa, hapo ndipo “kile kilicho kamili” kingekuja. Kwa hiyo, kwa wazi hilo halizungumzii muda ambao ‘zawadi ya lugha’ ingeendelea.

      Hata hivyo, Biblia inaonyesha muda ambao ‘zawadi ya lugha’ ingekuwa sehemu ya maisha ya Wakristo. Kulingana na maandishi, watu walipokea zawadi hiyo na zawadi nyingine za roho kwa kuwekewa mikono na mitume wa Yesu Kristo au mitume hao wakiwapo. (Mdo. 2:4, 14, 17; 10:44-46; 19:6; ona pia Mdo. 8:14-18.) Basi, baada ya kufa kwao na wakati watu waliokuwa wamepokea zawadi hizo kwa njia hiyo walipokufa, zawadi za kimuujiza zinazotokana na utendaji wa roho ya Mungu bila shaka zilikoma. Maoni hayo yanapatana na kusudi la zawadi hizo kama ilivyoandikwa katika Waebrania 2:2-4.

      Je, andiko la Marko 16:17, 18 (UV) linaonyesha kwamba uwezo wa ‘kusema kwa lugha mpya’ ungekuwa ishara ya kuwatambulisha waamini?

      Inafaa kukumbuka kwamba mistari hiyo haitaji tu ‘kusema kwa lugha mpya’ bali pia kushika nyoka na kunywa sumu inayoua. Je, wote ‘wanaosema kwa lugha’ wanawatia watu moyo wafanye mambo hayo pia?

      Ili kupata maelezo kuhusu sababu zinazowafanya wasomi wengine wa Biblia wasiikubali mistari hiyo, ona ukurasa wa 357, 358, chini ya kichwa, “Uponyaji.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki