Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uponyaji
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Je, maponyo ya leo yenye kusisimua yanafanywa kwa njia ileile kama maponyo ya kimuujiza yaliyofanywa na Yesu na wanafunzi wake wa kwanza?

      Malipo: “Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, fukuzeni roho waovu. Mlipokea bure, toeni bure.” (Mt. 10:8) (Je, waponyaji leo wanafanya hivyo—wanatoa bure, kama Yesu alivyoamuru?)

      Kiwango cha mafanikio: “Umati wote ulikuwa ukitafuta kumgusa, kwa sababu nguvu zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.” (Luka 6:19) “Wakawaleta wagonjwa nje hata katika zile njia pana na kuwalaza huko juu ya vitanda na machela, ili, wakati Petro anapopita hapo, angalau kivuli chake kipate kumwangukia mtu fulani kati yao. Pia, umati kutoka kwenye majiji yanayozunguka Yerusalemu ukazidi kuja pamoja, ukiwa umewabeba wagonjwa na wale wenye kutaabika wakiwa na roho wachafu, nao wote wakawa wakiponywa.” (Mdo. 5:15, 16) (Katika siku zetu, je, wote wanaowaendea waponyaji wa kidini au wanaoenda kwenye mahekalu ya kidini wakitafuta kuponywa, huponywa?)

      Je, maisha ya wafuasi wa mashirika ambayo “waponyaji” wanashirikiana nayo yanaonyesha kwamba wana roho ya Mungu?

      Wakiwa kikundi, je, wanaonyesha waziwazi matunda ya roho kama vile upendo, ustahimilivu, upole, kujizuia?—Gal. 5:22, 23.

      Je, kwa kweli wao “si sehemu ya ulimwengu,” wakiepuka kujiingiza katika siasa zote za ulimwengu? Je, wamejiepusha kabisa na hatia ya damu wakati wa vita? Je, wana sifa nzuri kwa sababu ya kuepuka mwenendo usio wa adili wa ulimwengu?—Yoh. 17:16; Isa. 2:4; 1 The. 4:3-8.

  • Uponyaji
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kwa nini Wakristo wa karne ya kwanza walipewa zawadi hizo, kama vile uwezo wa kuponya kimuujiza?

      Ebr. 2:3, 4: “Tutaponaje ikiwa tumepuuza wokovu mkuu namna hii kwa kuwa ulianza kusemwa kupitia Bwana wetu nasi tukathibitishiwa na wale waliomsikia, huku Mungu akijiunga katika kutoa ushahidi kwa ishara na vilevile mambo ya ajabu na matendo mbalimbali yenye nguvu na kwa ugawaji wa roho takatifu kulingana na mapenzi yake?” (Huo ulikuwa uthibitisho wenye kusadikisha, kwamba kutaniko la Kikristo, ambalo wakati huo lilikuwa jipya, lilikuwa la Mungu kikweli. Lakini mara tu lilipoimarishwa kikamili, je, ingekuwa lazima kuthibitisha jambo hilo tena na tena?)

      1 Kor. 12:29, 30; 13:8, 13: “Je, wote ni manabii? . . . Je, wote wana zawadi za maponyo? Je, wote husema kwa lugha? . . . Upendo haushindwi kamwe. Lakini kama kuna zawadi za kutoa unabii, zitaondolewa mbali; kama kuna lugha, zitakoma . . . Sasa, hata hivyo, inabaki imani, tumaini, upendo, hayo matatu; lakini lililo kubwa zaidi kati ya hayo ni upendo.” (Wakati zilipokuwa zimetimiza kusudi lake, zawadi hizo za kimuujiza zingekoma. Lakini sifa bora ambazo ni tunda la roho ya Mungu bado zingeonyeshwa katika maisha ya Wakristo wa kweli.)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki