Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Kristo Anapaswa Kukumbukwaje?
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Desemba 15
    • Ni kweli kwamba kuzaliwa kwa Yesu kulikuwa muhimu sana, lakini wanafunzi wake wa kwanza walitilia maanani yale ambayo alifanya na kufundisha. Bila shaka, Mungu hakukusudia kamwe kuzaliwa kwa Kristo kufanye maisha yake akiwa mtu mzima yapoteze umaana. Hata hivyo, Krismasi na hekaya zake za Mandhari ya Kuzaliwa kwa Yesu zimefanya Kristo apoteze umaana.

      Swali lingine lenye kusumbua linajitokeza kuhusiana na jinsi Krismasi inavyosherehekewa. Ikiwa Yesu angerudi duniani leo, angefikiri nini kuhusu jinsi ambavyo Krismasi imefanywa kuwa biashara ya waziwazi? Miaka elfu mbili iliyopita, Yesu alitembelea hekalu huko Yerusalemu. Alikasirishwa sana kuona wabadili-fedha na wachuuzi wakitumia vibaya sherehe za dini ya Kiyahudi ili kujifaidi. Alisema hivi: “Ondoeni vitu hivi kutoka hapa! Acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!” (Yohana 2:13-16) Kwa wazi, Yesu hakukubali kuchanganya biashara na dini.

  • Yesu Kristo Anapaswa Kukumbukwaje?
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Desemba 15
    • Mtoto Amezaliwa Kwetu

      Ikiwa desturi za Krismasi hazihusiani kabisa na Kristo, basi Wakristo wa kweli wanapaswa kukumbukaje kuzaliwa na maisha ya Kristo? Karne saba kabla ya kuzaliwa kwa Yesu, Isaya alitabiri hivi kumhusu: “Kuna mtoto ambaye amezaliwa kwetu, kuna mwana ambaye tumepewa; na utawala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake.” (Isaya 9:6) Kwa nini Isaya alionyesha kwamba kuzaliwa kwa Yesu na daraka ambalo angetimiza baadaye yangekuwa mambo muhimu? Kwa sababu Yesu angekuwa mtawala mwenye nguvu. Angeitwa Mkuu wa Amani, na amani au utawala wake wa kifalme haungekuwa na mwisho. Isitoshe, utawala wa Yesu ungetegemezwa “kwa njia ya haki na kwa njia ya uadilifu.”—Isaya 9:7.

      Malaika Gabrieli alirudia maneno ya Isaya wakati alipomtangazia Maria kuzaliwa kwa Yesu ambako kulikuwa kunakaribia. Alitabiri hivi: “Huyo atakuwa mkuu naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi; na Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, naye atatawala akiwa mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (Luka 1:32, 33) Bila shaka, kuzaliwa kwa Yesu kulikuwa muhimu kwa sababu kulihusiana na kazi ambayo Kristo angetimiza akiwa Mfalme aliyewekwa rasmi wa Ufalme wa Mungu. Utawala wa Kristo unaweza kuwafaidi watu wote, kutia ndani wewe na wapendwa wako. Kwa kweli, malaika walionyesha kwamba kuzaliwa kwake kungeleta “salama duniani, katika watu wanaomupendeza [Mungu].”—Luka 2:14, Zaire Swahili Bible.

      Sote tunatamani kuishi katika ulimwengu wenye amani na haki. Lakini ili kufurahia amani ambayo utawala wa Kristo utaleta, tunahitaji kumpendeza Mungu na kuwa na uhusiano mzuri pamoja naye. Yesu alisema kwamba hatua ya kwanza inayoongoza kwenye uhusiano huo ni kujifunza juu ya Mungu na Kristo. “Uzima wa milele ndio huu,” Yesu alisema, “waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”—Yohana 17:3.

      Tunapokuwa na ujuzi sahihi kumhusu Yesu, hatutahangaika tena kujua jinsi angependa tumkumbuke. Je, tungemkumbuka kwa kula, kunywa, na kupeana zawadi tarehe ileile ya sherehe ya kale ya kipagani? Yaelekea hangetaka tumkumbuke kwa njia hiyo? Usiku uliotangulia kifo chake, Yesu aliwaambia wanafunzi wake yale aliyotaka. “Yule aliye na amri zangu na kuzishika, huyo ndiye ambaye hunipenda. Naye anayenipenda atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda.”—Yohana 14:21.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki