-
Ukweli Kuhusu KrismasiAmkeni!—2010 | Desemba
-
-
Biblia inasema nini: Biblia haitaji tarehe ambayo Yesu alizaliwa. Lakini tunaweza kusema kwamba hakuzaliwa Desemba 25. Kwa nini? Biblia inatuambia kwamba Yesu alipozaliwa, wachungaji walikuwa “wakiishi nje” wakichunga makundi yao usiku karibu na Bethlehemu. (Luka 2:8) Kwa kawaida, majira ya baridi na mvua yalianza Oktoba (Mwezi wa 10), na mwezi wa Desemba ndio uliokuwa na baridi kali zaidi ambayo nyakati nyingine iliandamana na theluji. Wachungaji—hasa wale waliokuwa katika nyanda za juu zenye baridi, kama zile karibu na Bethlehemu—waliingiza kondoo wao katika vibanda usiku.a
Inafaa kuzingatia kwamba Wakristo wa mapema, ambao wengi wao walikuwa wameshirikiana na Yesu katika huduma yake, hawakuwahi kusherehekea kuzaliwa kwake katika tarehe yoyote. Badala yake, kupatana na amri yake, waliadhimisha tu kifo chake. (Luka 22:17-20; 1 Wakorintho 11:23-26) Lakini, bado huenda wengine wakasema, ‘Je, kuna ubaya wowote kwa Wakristo kuanza kufuata desturi za kipagani?’ Jibu? Kwa Mungu kuna ubaya. “Waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho na kweli,” akasema Yesu Kristo.—Yohana 4:23.
-
-
Ukweli Kuhusu KrismasiAmkeni!—2010 | Desemba
-
-
Biblia inasema nini: Biblia haisemi ni mamajusi wangapi waliomtembelea Yesu. Huenda walikuwa wawili, au huenda walikuwa watatu, wanne, au zaidi. Ingawa katika Biblia fulani wanaitwa “wanaume wenye hekima,” neno lililotumiwa katika lugha ya awali ni magoi, linalomaanisha wanajimu au walozi—kazi ambazo Biblia inasema ni “chukizo kwa Yehova.” (Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Kwa kuwa walisafiri mbali sana kutoka Mashariki, wanajimu hao hawakuwasili kwa wakati kumtembelea Yesu akiwa katika zizi. Badala yake, baada ya kusafiri kwa miezi mingi, walienda kwenye “nyumba” ambako Yesu alikuwa akiishi. Huko walimwona “mtoto mchanga pamoja na Maria mama yake.”—Mathayo 2:11.
-
-
Ukweli Kuhusu KrismasiAmkeni!—2010 | Desemba
-
-
Kwa wazi, hiyo haikuwa nyota ya kawaida! Kwa nini Mungu, ambaye alikuwa ametumia malaika kuwajulisha wachungaji wa hali ya chini kuhusu kuzaliwa kwa Yesu, atumie nyota kuongoza wanajimu wapagani—kwanza kwa adui ya Yesu kisha kwa mtoto mwenyewe? Inapatana na akili kusema kwamba nyota hiyo ilikuwa mbinu ya Shetani, anayeweza kujitokeza katika njia kama hizo. (2 Wathesalonike 2:9, 10) Jambo la kushangaza ni kwamba nyota inayoitwa ya Bethlehemu huwekwa juu kabisa ya mti wa Krismasi.
-
-
Ukweli Kuhusu KrismasiAmkeni!—2010 | Desemba
-
-
Biblia inasema nini: “Sasa kwa kuwa mmeuondolea mbali uwongo, semeni kweli kila mmoja wenu na jirani yake.” ‘Majirani’ wetu wa karibu zaidi ni watu wa familia yetu. (Waefeso 4:25) Pia Biblia inasema kwamba tunapaswa ‘kupenda kweli,’ “kusema kweli katika moyo [wetu].” (Zekaria 8:19; Zaburi 15:2) Ni kweli kwamba huenda ikaonekana kuwa hakuna madhara kuwaambia watoto kuwa Baba Krismasi (au Kristo mtoto) ndiye huwaletea zawadi wakati wa Krismasi, lakini je, ni jambo linalofaa kuwadanganya watoto wadogo, hata usipokuwa na nia mbaya? Je, si jambo la ajabu kwamba siku inayopaswa kumtukuza Yesu imekuwa siku ya kuwadanganya watoto?
-
-
Ukweli Kuhusu KrismasiAmkeni!—2010 | Desemba
-
-
Biblia inasema nini: Shangwe na ukarimu ni sehemu muhimu ya ibada ya kweli. Biblia inasema: ‘Iweni na shangwe, enyi waadilifu; na mpige vigelegele vya shangwe.’ (Zaburi 32:11) Mara nyingi, shangwe ya aina hiyo inahusianishwa na ukarimu. (Methali 11:25) Yesu Kristo alisema: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Pia alisema hivi: “Muwe na mazoea ya kuwapa watu,” yaani, tunapaswa kuhakikisha kwamba hilo ni jambo la kawaida katika maisha yetu.—Luka 6:38.
Kutoa kwa njia hiyo hakuna uhusiano na kutoa kidesturi au kutoa kwa kulazimishwa, kwa sababu tu ni zoea katika jamii. Biblia inasema hivi ikifafanua roho ya kweli ya kutoa: “Kila mmoja, basi, na atoe kadiri alivyoamua, kwa moyo na wala si kwa huzuni au kwa kulazimishwa, maana Mungu humpenda yule mwenye kutoa kwa furaha.” (2 Wakorintho 9:7, Biblia Habari Njema) Wale wanaotii kanuni hizo nzuri za Biblia hutoa kwa sababu moyo wao wenye ukarimu unawachochea kufanya hivyo, na wanatoa wakati wowote katika mwaka. Kwa kweli, Mungu hubariki kutoa kwa njia hiyo, na kufanya hivyo si mzigo mzito.
Sherehe Bandia!
Inapochunguzwa kwa kutumia Biblia, ni kana kwamba kila kitu kuhusu Krismasi kimetokana na mambo ya kipagani au kupotoshwa kwa masimulizi ya Biblia. Kwa hiyo, desturi za Krismasi zinaitwa tu za Kikristo. Basi zilianza jinsi gani kuitwa hivyo? Karne kadhaa baada ya kifo cha Kristo, walimu wengi wa uwongo walitokea, kama Biblia ilivyokuwa imetabiri. (2 Timotheo 4:3, 4) Watu hao wasioongozwa na kanuni walipendezwa zaidi na kufanya Ukristo upendwe na wapagani kuliko walivyopendezwa na kufundisha kweli. Kwa sababu hiyo, walianza kujiingiza hatua kwa hatua katika sherehe za dini za kipagani zilizopendwa sana na wakaziita eti ni za Kikristo.
Biblia ilionya kwamba ‘walimu hao wa uwongo watawatumia watu vibaya kwa maneno yasiyo ya kweli. Lakini kuwahusu wao, hukumu ya tangu zamani za kale haisongi polepole, na maangamizi yao hayalali.’ (2 Petro 2:1-3)
-