Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Anakuja Pamoja na Mawingu”

      6. (a) Yohana anatangaza nini kuhusu Yesu ‘akija pamoja na mawingu’ na Yohana huenda akawa alikumbushwa unabii gani wa Yesu? (b) Yesu ‘anakujaje,’ na ni nani wataona kihoro kikubwa duniani?

      6 Halafu, Yohana anatangaza kwa shangwe hivi: “Tazama! Yeye anakuja pamoja na mawingu, na kila jicho litaona yeye, na wale ambao walidunga yeye; na makabila yote ya dunia yatajipigapiga kwa kihoro kwa sababu yake yeye. Ndiyo, Ameni.” (Ufunuo 1:7, NW) Pasipo shaka Yohana alikumbushwa hapa unabii wa mapema zaidi wa Yesu kuhusu umalizio wa mfumo wa mambo. Wakati huo Yesu alitaarifu hivi: “Ndipo ishara ya Mwana wa binadamu itaonekana katika mbingu, na ndipo makabila yote ya dunia yatajipiga kwa maombolezo, na wataona Mwana wa binadamu akiwa anakuja juu ya mawingu ya mbingu kwa nguvu na utukufu mkubwa.” (Mathayo 24:3, 30, NW)

  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Yesu “anakuja pamoja na mawingu” katika maana ya kwamba yeye atakuwa asiyeonekana kwa jicho tupu kama vile jua linavyokuwa likiwa nyuma ya mawingu. Hata wakati jua linapofichwa na mawingu wakati wa mchana, sisi tunajua lipo kwa sababu ya nuru ya mchana inayotuzunguka. Vivyo hivyo, ingawa Bwana Yesu haonekani, yeye atafunuliwa kama ‘moto wenye kuwaka mwali, aletapo kisasi juu ya wale ambao hawatii habari njema kuhusu yeye.’ Hawa pia watalazimishwa ‘kuona yeye.’—1 Wathesalonike 1:6-8, NW; 2:8.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki