-
Kurudi kwa KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Tunapaswa kukumbuka kwamba kuna tofauti kati ya kuja na kuwapo. Kwa hiyo, ingawa kuja kwa mtu (kunakohusianishwa na kufika au kurudi kwake) kunatukia katika wakati fulani, huenda kuwapo kwake baada ya hapo kukaendelea kwa kipindi cha miaka kadhaa.
-
-
Kurudi kwa KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Katika Mathayo 24:37 neno la Kigiriki pa·rou·siʹa linatumiwa. Kihalisi maana yake ni “kuwa kando ya.” Kamusi Greek-English Lexicon (Oxford, 1968) ya Liddell na Scott inatoa “kuwapo, kwa watu,” kuwa maana ya kwanza ya pa·rou·siʹa. Maana ya neno hilo inaonyeshwa waziwazi katika Wafilipi 2:12, ambapo Paulo anatofautisha kuwapo kwake (pa·rou·siʹa) na kutokuwapo kwake (a·pou·siʹa). Kwa upande mwingine, neno la Kigiriki er·khoʹme·non limetumiwa katika andiko la Mathayo 24:30, linalosema kuhusu “Mwana wa binadamu akija [kutimiza kazi aliyopewa na Yehova ya kuwaangamiza waovu kwenye vita vya Har–Magedoni] juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi.” Watafsiri fulani hutumia ‘kuja’ kwa maneno yote mawili ya Kigiriki, lakini wale walio waangalifu zaidi huonyesha tofauti kati ya maneno hayo mawili.
-