Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwapo Kwa Kristo—kunamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Februari 15
    • 3. Ni baadhi ya mambo gani yanayotukia wakati wa kuwapo kwa Yesu?

      3 Mitume waliuliza kuhusu “kuwapo” gani? Neno hilo limetafsiriwa kutokana na neno la Kigiriki pa·rou·siʹa.a Pa·rou·siʹa au kuwapo kwa Kristo, kulianza Yesu alipowekwa rasmi kuwa Mfalme mbinguni mwaka wa 1914, na kungali kunaendelea, na kunatia ndani ile “dhiki kuu,” wakati atakapokuja kuwaharibu waovu. (Mt. 24:21) Mambo mbalimbali yanatukia wakati wa kuwapo kwa Yesu, kama vile “siku za mwisho” za mfumo huu mbovu wa mambo, kukusanywa kwa wale waliochaguliwa, na kufufuliwa kwenye uhai wa kimbingu. (2 Tim. 3:1; 1 Kor. 15:23; 1 The. 4:15-17; 2 The. 2:1) Tunaweza kusema kwamba kipindi cha “umalizio wa mfumo wa mambo” (syn·teʹlei·a) kinaenda sambamba na kipindi kinachoitwa kuwapo kwa Kristo (pa·rou·siʹa).

  • Kuwapo Kwa Kristo—kunamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Februari 15
    • a Maana ya neno pa·rou·siʹa inaonyeshwa na 2 Wakorintho 10:10, 11 na Wafilipi 2:12 ambapo “kuwapo” na “kutokuwapo” kwa mtume Paulo kunatofautishwa. Kwa habari zaidi, ona Insight on the Scriptures, Buku la 2, ukurasa wa 676-679 au Étude perspicace des Écritures, Buku la 2, ukurasa wa 648-651.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki