Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Desemba 1
    • MFALME AMJENGEA YEH

      OVA NYUMBA

      (2 Mambo ya Nyakati 1:1–9:31)

      Yehova anampa Mfalme Sulemani maombi ya moyo wake, yaani, hekima, ujuzi, pamoja na utajiri na heshima. Mfalme anamjengea Yehova nyumba yenye utukufu huko Yerusalemu, na watu wana ‘shangwe na wanachangamka moyoni.’ (2 Mambo ya Nyakati 7:10) Sulemani anakuwa “mkuu katika utajiri na hekima kuliko wafalme wengine wote wa dunia.”—2 Mambo ya Nyakati 9:22.

      Baada ya kutawala Israeli kwa miaka 40, Sulemani ‘analala pamoja na mababu zake, na Rehoboamu mwana wake anaanza kutawala mahali pake.’ (2 Mambo ya Nyakati 9:31) Ezra hazungumzii kukengeuka kwa Sulemani kuhusiana na ibada ya kweli. Makosa anayotaja yanahusu tu jinsi mfalme anavyojipatia farasi wengi kutoka Misri bila kutumia hekima na kuoa binti ya Farao. Hivyo, mwandishi wa kitabu hicho anakazia sifa nzuri tu.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Desemba 1
    • MFUATANO WA WAFALME KATIKA UKOO WA DAUDI

      (2 Mambo ya Nyakati 10:1–36:23)

      Ufalme ulioungana wa Israeli unagawanyika katika sehemu mbili, yaani, ufalme wa kaskazini wa makabila kumi na ufalme wa kusini wa makabila mawili ya Yuda na Benyamini. Makuhani na Walawi katika Israeli yote wanaonyesha ushikamanifu wao kwa agano la Ufalme badala ya kuonyesha ushikamanifu kwa taifa, nao wanamuunga mkono Rehoboamu mwana wa Sulemani. Miaka 30 hivi baada ya kumaliza ujenzi wa hekalu, hazina ya hekalu inaibwa.

      Kati ya wafalme 19 ambao wanatawala baada ya Rehoboamu, 5 ni waaminifu, 3 wanaanza vizuri wakiwa waaminifu lakini baadaye wanakuwa wasio waaminifu, na mmoja anatubu na kuacha njia zake mbaya. Watawala wengine wote wanatenda yaliyo mabaya machoni pa Yehova.b Matendo ya wafalme watano ambao wanamtegemea Yehova yanakaziwa. Masimulizi yanayoeleza jinsi Hezekia alivyoanzisha tena huduma hekaluni na jinsi Yosia alivyofanya matayarisho kwa ajili ya Pasaka kuu yaliwatia moyo Wayahudi waliopendezwa na kurudishwa kwa ibada ya Yehova huko Yerusalemu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki