-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 681]
Maurice Duplessis, waziri mkuu wa Quebec, akipiga magoti hadharani mbele ya Kadinali Villeneuve mwishoni-mwishoni mwa miaka ya 1930 na kuweka pete kwenye kidole chake ukiwa uthibitisho wa uhusiano wa karibu kati ya Kanisa na Serikali. Katika Quebec, mnyanyaso wa Mashahidi wa Yehova ulikuwa mwingi hasa
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Hicho kilikuwa kipindi ambacho Kanisa la Katoliki ya Roma lilikuwa na uvutano mwingi ambao kila mwanasiasa na kila hakimu katika mkoa huo asingepuuza. Katika Quebec makasisi kwa kawaida walionwa kwa heshima kuu, na watu wengine walitii kwa utayari maneno ya padri mwenyeji. Kama vile kitabu State and Salvation (1989) kilivyoeleza hali hiyo: “Kadinali wa Quebec alikuwa na kiti kikuu Bungeni kando tu ya kile cha mkuu wa serikali. Kwa njia moja au nyingine sehemu kubwa ya Quebec ilikuwa chini ya udhibiti wa moja kwa moja wa kanisa . . . Kwa kweli, lengo la kanisa lilikuwa ni kufanya hali ya kisiasa ya Quebec ipatane na wazo la Katoliki ya Roma ambalo kwalo kweli ni Ukatoliki, kosa ni chochote kisicho cha Ukatoliki, na uhuru ni kutozuiwa kusema na kuishi kulingana na kweli ya Katoliki ya Roma.”
-