Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko
    Huduma ya Ufalme—2004 | Agosti
    • Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko

      Ulimwengu wa Shetani unapozidi kuzorota, Yehova anatutia nguvu ili ‘tukatae kabisa kutomwogopa Mungu na tamaa za kilimwengu na tuishi kwa utimamu wa akili na uadilifu na ujitoaji-kimungu katikati ya mfumo wa mambo wa sasa.’ (Tito 2:12) Baadhi ya mipango ambayo anafanya kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ni makusanyiko ya mzunguko na makusanyiko ya pekee. (Mt. 24:45) Tunaimarishwa sana katika makusanyiko haya ya kiroho!

      Ili tusaidiwe kutumia maishani mwetu mafundisho tunayopokea, tutatumia mpango mpya wa kupitia habari za makusanyiko hayo katika mwaka wa utumishi wa 2005. Katika ukurasa wa 5 na 6 wa nyongeza hii kuna makala zinazoonyesha mambo yatakayozungumziwa kwenye makusanyiko hayo na vilevile maswali ya kupitia programu za makusanyiko hayo. Makutaniko yatazungumzia habari hizo kwenye Mkutano wa Utumishi muda mfupi kabla na baada ya kuhudhuria makusanyiko yao. Mapitio hayo yatapangwaje?

      Juma moja au mawili kabla kutaniko halijahudhuria kusanyiko la mzunguko, hotuba ya dakika kumi inayotegemea makala “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko” itatolewa kwenye Mkutano wa Utumishi ili kuwatia ndugu hamu ya kusikiliza programu. Msemaji atataja pia maswali ya kupitia na kuwatia wote moyo waandike mambo makuu ili wawe tayari kwa ajili ya pitio litakalofanywa majuma machache baada ya kusanyiko.

      Majuma machache baada ya kusanyiko, muda wa dakika 15 utatumiwa kupitia programu ya siku ya kwanza ya kusanyiko katika Mkutano wa Utumishi. Juma linalofuata, dakika 15 zitatumiwa kupitia programu ya siku ya pili ya kusanyiko. Mazungumzo hayo yatategemea maswali ya kupitia yanayopatikana katika nyongeza hii. Pitio hilo linapaswa kukazia hasa jinsi tunavyoweza kutumia habari hizo maishani mwetu. Ili kupata nafasi ya kufanya mapitio hayo, wazee wanapaswa kufupisha au kufuta sehemu nyingine za Mkutano wa Utumishi, au kupanga zishughulikiwe juma lingine.

  • Pitio La Kusanyiko La Mzunguko
    Huduma ya Ufalme—2004 | Agosti
    • Pitio La Kusanyiko La Mzunguko

      Makala hii itatumiwa kupitia programu ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 2005, kabla na baada ya kusanyiko. Makala yenye kichwa, “Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko,” kwenye ukurasa wa 4 katika nyongeza hii, inaeleza jinsi ya kufanya mapitio hayo. Maswali yote yanapaswa kuzungumziwa wakati wa pitio litakalofanywa baada ya kusanyiko. Pitio linapaswa kukazia jinsi tunavyoweza kutumia maishani mwetu mambo tuliyojifunza kusanyikoni.

      KIPINDI CHA ASUBUHI SIKU YA KWANZA

      1. Ni nini kitakachotusaidia kupata hekima ya Mungu?

      2. Ndugu na dada katika mzunguko wamefanya jitihada gani ili kuwapata watu wengi zaidi ili wawahubirie habari njema?

      KIPINDI CHA ALASIRI SIKU YA KWANZA

      3. Kwa nini ni muhimu kwa Mkristo awe safi kiakili na kiroho? Tunaweza kufaulu jinsi gani kuwa safi kiakili na kiroho?

      4. Tunaweza kujionyesha kuwa wenye kufanya amani jinsi gani tunaposhirikiana na ndugu zetu?

      5. Usawaziko ni nini, na tunawezaje kuonyesha sifa hiyo tunapotenga wakati ili tutimize wajibu mbalimbali?

      6. Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Sauli na Noa? Tunaweza kuonyesha kwa njia zipi kwamba sisi tuko “tayari kutii”? (Yakobo 3:17)

      7. Wakristo wanaweza kujihadhari jinsi gani wasiishi maisha maradufu?

      8. Tunawezaje kusema hekima ya Mungu kama Paulo?

      KIPINDI CHA ASUBUHI SIKU YA PILI

      9. Kwa nini tunapaswa kuchagua mambo tunayotaka kufuatia kwa busara, na ni nini kitakachotusaidia kufanya maamuzi mazuri?

      10. Ndugu na dada katika mzunguko wanafanya jitihada gani ili kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, nao wamenufaikaje kwa kufanya hivyo?

      11. Vichwa wa familia wanawezaje kuwaimarisha kiroho watu wa familia zao?

      12. Tuliarifiwa kuhusu mahitaji gani ya mzunguko?

      KIPINDI CHA ALASIRI SIKU YA PILI

      13. Kama hotuba ya watu wote ilivyoonyesha, hekima kutoka juu imechochea matendo gani ya uadilifu?

      14. Kwa nini ni upumbavu kujitegemea au kuwategemea wale wasioongozwa na hekima ya Mungu? Sisi tunapaswa kujihadhari kuhusiana na mambo gani?

      15. Hekima ya Mungu hutulinda na mitego gani?

      16. Kwa nini ni muhimu kwetu kufuata ushauri tuliopokea kwenye kusanyiko la mzunguko?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki