-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Miaka mingi baadaye, katika kitabu Preachers Present Arms, Dakt. Ray Abrams alionelea hivi: “Ni jambo lenye kutokeza kwamba makasisi wengi walishiriki sehemu ya uchochezi katika kujaribu kuwaondolea mbali Warusselli [kama vile Wanafunzi wa Biblia walivyoitwa kwa dharau]. Mizozo ya kidini na chuki za muda mrefu, ambazo hazikushughulikiwa kwa vyovyote mahakamani katika wakati wa amani, sasa zilifika mahakamani chini ya uvutano wa harara ya wakati wa vita.” Yeye pia alisema: “Uchanganuzi wa kesi yote huongoza kwenye mkataa kwamba hapo awali makanisa na makasisi walichochea harakati ya kuwafutilia mbali Warusselli.”—Kur. 183-185.
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
◆ Dakt. Ray Abrams, katika kitabu chake “Preachers Present Arms,” alionelea hivi: “Wakati habari za hukumu ya vifungo hivyo vya miaka ishirini zilipofikia wahariri wa magazeti ya kidini, karibu kila kimoja cha vichapo hivyo, kikubwa na kidogo, kilishangilia tukio hilo. Mimi nimeshindwa kupata maneno yoyote ya masikitiko katika yoyote ya majarida ya kidini yanayokubaliwa.”
-