-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Miaka mingi baadaye, katika kitabu Preachers Present Arms, Dakt. Ray Abrams alionelea hivi: “Ni jambo lenye kutokeza kwamba makasisi wengi walishiriki sehemu ya uchochezi katika kujaribu kuwaondolea mbali Warusselli [kama vile Wanafunzi wa Biblia walivyoitwa kwa dharau]. Mizozo ya kidini na chuki za muda mrefu, ambazo hazikushughulikiwa kwa vyovyote mahakamani katika wakati wa amani, sasa zilifika mahakamani chini ya uvutano wa harara ya wakati wa vita.” Yeye pia alisema: “Uchanganuzi wa kesi yote huongoza kwenye mkataa kwamba hapo awali makanisa na makasisi walichochea harakati ya kuwafutilia mbali Warusselli.”—Kur. 183-185.
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 655]
Makasisi Waonyesha Hisia Zao
Maitikio ya magazeti ya kidini baada ya kuhukumiwa kwa J. F. Rutherford na washiriki wake mwaka 1918 yanastahili kuangaliwa:
◆ “The Christian Register”: “Kile ambacho Serikali hapa inashambulia moja kwa moja kwa njia ya kufisha ni ile dhana kwamba mawazo ya kidini, hata yawe ya kichaa na yenye kudhuru jinsi gani, yanaweza kuenezwa bila hofu ya kuadhibiwa. Dhana hiyo ni uwongo wa kale, na kufikia sasa hatujakuwa waangalifu sana kulihusu. . . . Hukumu hiyo inaonekana kuwa ndiyo mwisho wa Urusselli.”
◆ “The Western Recorder,” kichapo cha Baptisti, kilisema: “Haishangazi kwamba kiongozi wa kidhehebu hicho chenye ukaidi amefungiwa katika mojawapo ya vituo vya watu wakaidi. . . . Tatizo lenye kutatanisha kwelikweli kuhusiana na jambo hilo ni ikiwa washtakiwa wangepaswa wapelekwe kwenye makao ya wenye kichaa au kwenye gereza.”
◆ “The Fortnightly Review” lilielekeza fikira kwenye maelezo katika gazeti la New York “Evening Post,” ambalo lilisema: “Tunatumaini kwamba walimu wa dini kila mahali wataona maoni ya hakimu huyu kwamba kufunza dini yoyote isipokuwa ile ambayo inapatana kabisa na sheria zilizowekwa ni hatia kubwa ambayo inafanywa kuwa kubwa zaidi, ikiwa wewe ukiwa mhudumu wa gospeli, ungali mnyoofu.”
◆ “The Continent” kwa kuwashushia heshima liliwaonyesha washtakiwa kuwa “wafuasi wa ‘Pasta’ Russell aliyekufa” na likapotoa imani zao kwa kusema kwamba waliunga mkono “kwamba watu wote wanapaswa wasipelekwe kupigana na kaiser wa Ujerumani isipokuwa wale wenye dhambi.” Lilidai kwamba kulingana na wakili mkuu katika Washington, “muda fulani uliopita serikali ya Italia ililalamikia Marekani kwamba Rutherford na washiriki wake . . . walikuwa wameeneza kiasi fulani cha propaganda ya kupinga vita katika majeshi ya Italia.”
◆ Juma moja baadaye, “The Christian Century” lilichapa sehemu kubwa ya habari iliyo juu neno kwa neno, ikionyesha kwamba walikubaliana nayo kabisa.
◆ Gazeti la Katoliki “Truth” liliripoti kifupi ile hukumu waliyopewa na kisha likaeleza hisi za wahariri walo, likisema: “Fasihi za shirika hilo zimejaa mashambulizi makali sana juu ya Kanisa Katoliki na upadri walo.” Ili kujaribu kuweka kibandiko cha “uasi” juu ya yeyote ambaye huenda akapinga hadharani maoni ya Kanisa Katoliki, liliongezea hivi: “Inazidi kuwa wazi kwamba roho ya kutovumilia inafungamanishwa kwa ukaribu na ile ya uasi.”
◆ Dakt. Ray Abrams, katika kitabu chake “Preachers Present Arms,” alionelea hivi: “Wakati habari za hukumu ya vifungo hivyo vya miaka ishirini zilipofikia wahariri wa magazeti ya kidini, karibu kila kimoja cha vichapo hivyo, kikubwa na kidogo, kilishangilia tukio hilo. Mimi nimeshindwa kupata maneno yoyote ya masikitiko katika yoyote ya majarida ya kidini yanayokubaliwa.”
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Ni Nani kwa Kweli Aliyeyachochea?
Je, yote hayo kwa kweli yalichochewa na makasisi? John Lord O’Brian alikana hilo. Lakini mambo ya hakika yalijulikana vema na wale walioishi wakati huo. Katika Machi 22, 1919, gazeti lililochapwa katika Girard, Kansas liitwalo Appeal to Reason, liliteta hivi: “Wafuasi wa Pasta Russell, Wakifuatiwa na Ukorofi wa Makasisi wa ‘Orthodoksi,’ Walihukumiwa na Kufungwa Bila Dhamana, Ingawa Walifanya Kila Jitihada Iliyowezekana ili Kushikamana na Masharti ya Sheria ya Ujasusi.
-