Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Makasisi Waendelea Kupigana

      Kufuatia Vita ya Ulimwengu 2, makasisi katika sehemu ya mashariki mwa Chekoslovakia waliendelea kuchochea mnyanyaso wa Mashahidi wa Yehova. Wakati wa kipindi cha kukaliwa na Wanazi, walikuwa wameshtaki kwamba Mashahidi walikuwa Wakomunisti; sasa walidai kwamba Mashahidi walipinga serikali ya Ukomunisti. Nyakati nyingine, wakati Mashahidi wa Yehova walipozuru nyumba za watu, mapadri walihimiza walimu wawaache mamia ya watoto waondoke shuleni ili wakawarushie Mashahidi mawe.

      Vivyo hivyo, mapadri Wakatoliki katika Santa Ana, El Salvador, walifanya uchochezi dhidi ya Mashahidi katika 1947. Wakati ndugu walipokuwa na Funzo la Mnara wa Mlinzi la kila juma, wavulana walirusha mawe kupitia kwa mlango uliokuwa wazi. Kisha ukaja mwandamano ulioongozwa na mapadri. Wengine walibeba mianga; wengine walibeba mifano. “Bikira na aishi milele!” wakapaaza sauti. “Yehova na afe!” Kwa muda wa saa mbili hivi, jengo hilo lilipigwa kwa mawe.

      Katika miaka ya katikati ya 1940, Mashahidi wa Yehova katika Quebec, Kanada, walitendwa vibaya sana pia, mikononi mwa magenge ya Wakatoliki na maofisa vilevile. Wajumbe kutoka jumba kuu la askofu walienda kila siku kwenye idara ya polisi ili kudai kwamba polisi wawaondolee mbali Mashahidi. Mara nyingi, kabla ya mtu kukamatwa, polisi walionwa wakitokea mlango wa nyuma wa kanisa. Katika 1949, wamishonari wa Mashahidi wa Yehova walifukuzwa kutoka Joliette, Quebec, na magenge ya Wakatoliki.

  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Katika Sucre, Bolivia, kulikuwa na jeuri zaidi. Katika wakati wa kusanyiko la Mashahidi wa Yehova katika 1955, genge la wavulana kutoka Shule ya Katoliki ya Sacred Heart walizunguka mahali pa kusanyiko, wakapiga kelele, na kutupa mawe. Kutoka jengo la kanisa lililo upande ule mwingine wa barabara, kipaza sauti chenye nguvu kilihimiza Wakatoliki wote walinde kanisa lao na “Bikira” dhidi ya “washupavu Waprotestanti.” Askofu mkuu na mapadri walijaribu binafsi kuvunja mkutano huo lakini waliamriwa na polisi waondoke katika jumba hilo.

      Mwaka uliotangulia, wakati Mashahidi wa Yehova walipokuwa na kusanyiko jijini Riobamba, Ekuado, programu yao ilikuwa na hotuba ya watu wote yenye kichwa “Upendo, Unatumika Katika Ulimwengu Wenye Ubinafsi?” Lakini padri Myesuiti alikuwa amechochea Wakatoliki, akiwahimiza wazuie mkutano huo usifanyike. Hivyo, hotuba hiyo ilipoanza, genge lingeweza kusikika likipiga kelele: “Kanisa Katoliki na liishi milele!” na, “Waprotestanti chini!” Kwa shukrani polisi waliwazuia, panga zao zikiwa zimechomolewa. Lakini genge hilo lilitupa mawe katika sehemu ya mkutano na, baadaye, kwenye jengo ambamo wamishonari waliishi.

      Makasisi wa Katoliki ya Roma wamekuwa katika mstari wa mbele wa mnyanyaso, lakini si hao tu. Makasisi wa Orthodoksi ya Ugiriki wamekuwa wakali vivyo hivyo na wametumia mbinu zilezile katika eneo lao ndogo zaidi wanaloongoza. Kwa kuongezea, makasisi wengi Waprotestanti wameonyesha roho iyo hiyo mahali walipohisi kwamba wangeweza kuionyesha. Kwa kielelezo, katika Indonesia wameongoza magenge yaliyovunja mafunzo ya Biblia katika nyumba za faragha na ambayo yalipiga kikatili wale Mashahidi wa Yehova waliokuwapo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki