-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Makasisi Waendelea Kupigana
Kufuatia Vita ya Ulimwengu 2, makasisi katika sehemu ya mashariki mwa Chekoslovakia waliendelea kuchochea mnyanyaso wa Mashahidi wa Yehova. Wakati wa kipindi cha kukaliwa na Wanazi, walikuwa wameshtaki kwamba Mashahidi walikuwa Wakomunisti; sasa walidai kwamba Mashahidi walipinga serikali ya Ukomunisti. Nyakati nyingine, wakati Mashahidi wa Yehova walipozuru nyumba za watu, mapadri walihimiza walimu wawaache mamia ya watoto waondoke shuleni ili wakawarushie Mashahidi mawe.
Vivyo hivyo, mapadri Wakatoliki katika Santa Ana, El Salvador, walifanya uchochezi dhidi ya Mashahidi katika 1947. Wakati ndugu walipokuwa na Funzo la Mnara wa Mlinzi la kila juma, wavulana walirusha mawe kupitia kwa mlango uliokuwa wazi. Kisha ukaja mwandamano ulioongozwa na mapadri. Wengine walibeba mianga; wengine walibeba mifano. “Bikira na aishi milele!” wakapaaza sauti. “Yehova na afe!” Kwa muda wa saa mbili hivi, jengo hilo lilipigwa kwa mawe.
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika Sucre, Bolivia, kulikuwa na jeuri zaidi. Katika wakati wa kusanyiko la Mashahidi wa Yehova katika 1955, genge la wavulana kutoka Shule ya Katoliki ya Sacred Heart walizunguka mahali pa kusanyiko, wakapiga kelele, na kutupa mawe.
-