-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Makasisi Waendelea Kupigana
Kufuatia Vita ya Ulimwengu 2, makasisi katika sehemu ya mashariki mwa Chekoslovakia waliendelea kuchochea mnyanyaso wa Mashahidi wa Yehova. Wakati wa kipindi cha kukaliwa na Wanazi, walikuwa wameshtaki kwamba Mashahidi walikuwa Wakomunisti; sasa walidai kwamba Mashahidi walipinga serikali ya Ukomunisti. Nyakati nyingine, wakati Mashahidi wa Yehova walipozuru nyumba za watu, mapadri walihimiza walimu wawaache mamia ya watoto waondoke shuleni ili wakawarushie Mashahidi mawe.
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika miaka ya katikati ya 1940, Mashahidi wa Yehova katika Quebec, Kanada, walitendwa vibaya sana pia, mikononi mwa magenge ya Wakatoliki na maofisa vilevile. Wajumbe kutoka jumba kuu la askofu walienda kila siku kwenye idara ya polisi ili kudai kwamba polisi wawaondolee mbali Mashahidi. Mara nyingi, kabla ya mtu kukamatwa, polisi walionwa wakitokea mlango wa nyuma wa kanisa. Katika 1949, wamishonari wa Mashahidi wa Yehova walifukuzwa kutoka Joliette, Quebec, na magenge ya Wakatoliki.
-
-
“Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Hata hivyo, Kanisa Katoliki limetumia kila njia iwezekanayo ili kudumisha udhibiti imara wa watu. Kwa kuwakaza maofisa wa serikali, walihakikisha kwamba wamishonari Mashahidi waliamriwa waondoke Italia mwaka 1949 na kwamba, ilipowezekana, ruhusa zilizopatikana na Mashahidi kwa ajili ya makusanyiko huko zilifutwa wakati wa miaka ya 1950. Kujapokuwa hayo, idadi ya Mashahidi wa Yehova iliendelea kukua, na kufikia 1992 kulikuwa na Mashahidi waeneza-evanjeli zaidi ya 190,000 katika Italia.
Kama vile katika wakati wa Baraza la Kuwahukumu Wazushi wa Kidini, makasisi katika Hispania walishutumu kisha wakaachia Serikali iwashtaki Mashahidi. Kwa kielelezo, katika Barcelona, ambako askofu mkuu alianzisha kampeni dhidi ya Mashahidi katika 1954, makasisi walitumia mimbari zao pamoja na shule na redio ili kuwashauri watu kwamba wakati Mashahidi watakapowazuru, wanapaswa kuwaalika ndani—kisha kuwaita polisi upesi.
-