Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g97 9/22 uku. 32
  • Inarudisha Tumaini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Inarudisha Tumaini
  • Amkeni!—1997
Amkeni!—1997
g97 9/22 uku. 32

Inarudisha Tumaini

Hayo yalikuwa maneno ya mwanamume mmoja aliyepokea nakala ya kikaratasi chenye kurasa nne kiitwacho Habari za Ufalme. Kilikuwa na kichwa “Kwa Nini Maisha Yamejaa Matatizo Sana?” Barua ya mwanamume huyo kuhusu kikaratasi hicho ilichapishwa kwenye gazeti la habari la El Tiempo, la Bogotá, Kolombia. Yeye aliandika:

“Katika nyakati hizi ambapo kila kitu chaonekana kufanyika kwa matendo ya jeuri na ufisadi, tunapohisi kwamba tumaini letu linakwisha, inatupasa kutafuta kwa kadiri fulani mambo ya kiroho ili kusaidia kudumisha imani yetu. Hapa pana mambo makuu ya maandishi niliyopewa:

“‘Biblia yafunua kwamba Mungu ataingilia mambo ya binadamu akitumia serikali yake ya kimbingu iliyo mikononi mwa Yesu Kristo. Ufalme huu utavunja vipande vipande serikali zote zenye ufisadi kutoka kwenye sayari. Je, wengine wataokoka mwisho wa huu ulimwengu? Waokokaji hawa wataishi milele wapi? Wenye haki watairithi nchi. Katika ulimwengu mpya wa Mungu, kifo hakitakuwapo tena. Hakutakuwa na uhalifu, umaskini, njaa, ugonjwa, kilio, wala kifo. Wafu watafufuliwa, na dunia itageuzwa iwe paradiso halisi.’”

Mashahidi wa Yehova wanafurahi kutoa msaada kwa wale wanaotaka kukua katika ujuzi wa Biblia. Ikiwa ungependa kupokea habari zaidi, tafadhali andikia I.B.S.A. Box 47788, Nairobi, au tumia anwani iliyo karibu zaidi nawe iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki