Inarudisha Tumaini
Hayo yalikuwa maneno ya mwanamume mmoja aliyepokea nakala ya kikaratasi chenye kurasa nne kiitwacho Habari za Ufalme. Kilikuwa na kichwa “Kwa Nini Maisha Yamejaa Matatizo Sana?” Barua ya mwanamume huyo kuhusu kikaratasi hicho ilichapishwa kwenye gazeti la habari la El Tiempo, la Bogotá, Kolombia. Yeye aliandika:
“Katika nyakati hizi ambapo kila kitu chaonekana kufanyika kwa matendo ya jeuri na ufisadi, tunapohisi kwamba tumaini letu linakwisha, inatupasa kutafuta kwa kadiri fulani mambo ya kiroho ili kusaidia kudumisha imani yetu. Hapa pana mambo makuu ya maandishi niliyopewa:
“‘Biblia yafunua kwamba Mungu ataingilia mambo ya binadamu akitumia serikali yake ya kimbingu iliyo mikononi mwa Yesu Kristo. Ufalme huu utavunja vipande vipande serikali zote zenye ufisadi kutoka kwenye sayari. Je, wengine wataokoka mwisho wa huu ulimwengu? Waokokaji hawa wataishi milele wapi? Wenye haki watairithi nchi. Katika ulimwengu mpya wa Mungu, kifo hakitakuwapo tena. Hakutakuwa na uhalifu, umaskini, njaa, ugonjwa, kilio, wala kifo. Wafu watafufuliwa, na dunia itageuzwa iwe paradiso halisi.’”
Mashahidi wa Yehova wanafurahi kutoa msaada kwa wale wanaotaka kukua katika ujuzi wa Biblia. Ikiwa ungependa kupokea habari zaidi, tafadhali andikia I.B.S.A. Box 47788, Nairobi, au tumia anwani iliyo karibu zaidi nawe iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.