-
Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni PoteMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika Barranquilla, Kolombia, wakati Olaf Olson alipotoa ushahidi kwa Antonio Carvajalino, aliyekuwa muungaji mkono mshupavu wa chama fulani cha kisiasa, Ndugu Olson hakumuunga mkono wala hakupendekeza wazo lolote lile la kisiasa. Badala yake, alijitoa kujifunza Biblia na Antonio na dada zake bila malipo. Upesi Antonio aling’amua kwamba kwa kweli Ufalme wa Mungu ndio tumaini pekee kwa watu maskini wa Kolombia na ulimwengu wote. (Zab. 72:1-4, 12-14; Dan. 2:44) Antonio na dada zake wakawa watumishi wa Mungu wenye bidii.
-
-
Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni PoteMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika sehemu nyingine wamishonari Mashahidi walilazimika kufanya kazi ya kimwili kwa wakati fulani ili tu kujiwekea msingi katika nchi fulani ndipo waweze kuendelea na huduma yao huko. Hivyo, wakati Jesse Cantwell alipoenda Kolombia, alifundisha Kiingereza katika idara ya utabibu ya chuo kikuu hadi hali ya kisiasa ilipobadilika na vizuizi vya kidini vikaondolewa. Baada ya hapo aliweza kutumia ujuzi wake katika huduma ya wakati wote akiwa mwangalizi asafiriye wa Mashahidi wa Yehova.
-