-
“Kutafuta Kwanza Ufalme”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Ili kuwasaidia na gharama za usafiri, chakula, mavazi, na makao, Zion’s Watch Tower Tract Society iliwapa makolpota hao wa mapema fasihi za Biblia ili wazigawanye, ikataarifu mchango wa kiasi ambao ungeweza kuombwa kwa ajili ya fasihi, na kuwaalika makolpota watumie sehemu ya fedha zilizopokewa.
-
-
“Kutafuta Kwanza Ufalme”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kushughulikia Mahitaji ya Kimwili
Walishughulikiaje mahitaji yao ya kimwili? Anna Petersen (baadaye Rømer), mweneza-evanjeli wa wakati wote katika Denmark, akumbuka: “Tulipata msaada kutoka kwa fasihi tulizoangusha ili kulipia gharama za kila siku, na mahitaji yetu hayakuwa makubwa. Kulipokuwa na gharama kubwa zaidi, hizo zililipiwa kwa njia moja au nyingine. Dada walikuwa wakitupatia nguo, marinda au makoti, na tungeyavaa mara hiyo, na hivyo tulivalia vizuri. Na katika nyakati fulani za baridi kali, nilifanya kazi ya ofisi kwa miezi kadhaa. . . . Kwa kununua mavazi wakati bei zilipokuwa chini, ningeweza kununua nguo nilizohitaji za mwaka mzima. Mambo yalienda sawa. Hatukuwa kamwe na uhitaji.” Vitu vya kimwili havikuwa hangaiko lao kuu. Upendo wao kwa Yehova na njia zake ulikuwa kama moto uwakao ndani yao, na ilikuwa lazima wauonyeshe tu.
Ili kupata malazi, wangekodi chumba kidogo huku wakihubiria watu katika eneo hilo. Wengine wao walitumia trela—kitu sahili, mahali tu pa kulala na kulia. Wengine walilala katika mahema na kuhamahama. Mahali pengine, ndugu walipanga kuwa na “kambi za mapainia.” Huenda Mashahidi katika eneo hilo wakaandaa makao, na mtu mmoja angegawiwa kuyasimamia. Mapainia waliotumikia katika eneo hilo wangeweza kutumia makao hayo, na wangeshiriki kulipa gharama zilizohusika.
Wafanyakazi hao wa wakati wote hawakuruhusu ukosefu wa pesa uwazuie watu wenye mfano wa kondoo kupata fasihi za Biblia. Mara nyingi mapainia walibadilishana fasihi kwa mazao kama viazi, siagi, mayai, matunda yaliyotoka kuchumwa au ya mkebe, kuku, sabuni na karibu kitu kingine chochote. Hawakuwa wanakuwa matajiri; badala yake, hiyo ilikuwa njia ya kuwasaidia watu wanyoofu wapate ujumbe wa Ufalme, hali wakati uleule wakipata mahitaji ya kimwili yaliyo ya lazima kwa maisha ili mapainia waweze kuendelea na huduma yao. Walikuwa na uhakika katika ahadi ya Yesu kwamba ikiwa ‘wangetafuta kwanza Ufalme na uadilifu wa Mungu,’ basi chakula na mavazi yanayohitajiwa yangeandaliwa.—Mt. 6:33, NW.
-