-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
HALI INABADILIKA
Baada ya kifo cha Lenin, serikali ilizidisha mashambulizi dhidi ya dini zote. Mnamo 1926, Shirika la Watu Wanaoamini Hakuna Mungu lilianzishwa. Jina la shirika hilo lilionyesha wazi makusudi yake. Propaganda za kwamba hakuna Mungu zilizoenezwa zilikusudiwa kuondoa kabisa katika mioyo na akili za watu imani katika Mungu. Punde si punde, imani ya kutokuwapo kwa Mungu ilienea kotekote katika eneo hilo kubwa la Muungano wa Sovieti. Mwanafunzi mmoja wa Biblia aliandika hivi katika barua aliyotuma kwenye makao makuu ya ulimwenguni pote: “Vijana wanakuwa na roho hiyo ya kutomwamini Mungu, na bila shaka hicho ni kizuizi kikubwa cha kujifunza kweli.”
Shirika hilo lilichapisha vichapo kuhusu kutokuwapo kwa Mungu, kutia ndani gazeti lililoitwa Antireligioznik. Mnamo 1928, gazeti hilo lilitangaza hivi: “Wilaya ya Voronezh imejaa madhehebu.” Kati ya madhehebu hayo, lilitaja ‘Wanafunzi 48 wa Maandiko Matakatifu’ ambao “viongozi wao walikuwa Zinchenko na Mitrofan Bovin.”
-
-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Wakati huohuo, Serikali mpya ya Sovieti haikuwa imetangaza waziwazi msimamo wake kuhusu dini. Hati mbalimbali za serikali zilionyesha kwamba serikali ilitaka vikundi vya kidini viwe sehemu ya wafanyakazi wa serikali. Katika miaka iliyofuata, serikali ilisisitiza jambo hilo. Ni jambo la maana kuelewa kwamba serikali ya Sovieti haikutaka kuwaua watu wa Yehova; ilitaka kugeuza akili na mioyo yao. Ilitaka kuwasadikisha watu wa Mungu watii sera za Kisovieti, kuwalazimisha wawe washikamanifu tu kwa Serikali. Haikutaka kamwe wawe waaminifu kwa Yehova.
-