Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ni Nani Anayeweza Kuwakomboa Wale Wanaolilia Msaada?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Agosti 15
    • Tuna kila sababu ya kuvutiwa na huruma nyingi ambayo aliwaonyesha watu waliokuwa wakiteseka. (Mt. 9:35, 36; 15:29-31) Kwa mfano, mtu fulani aliyekuwa akiteseka kwa sababu ya ukoma alimwendea Yesu na kumsihi hivi: “Ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.” Yesu akamjibu hivi: “Ninataka. Takasika.” Na mara moja mwanamume huyo akaponywa! (Marko 1:40-42) Baadaye, Yesu alikutana na mjane ambaye mwana wake wa pekee alikuwa amekufa. Yesu “akamsikitikia” na kusema, “Inuka!” na mwana wake akainuka. Akawa hai tena!—Luka 7:11-15.

      7, 8. Yesu alionyesha nguvu zake za kuponya katika njia gani mbalimbali?

      7 Yehova alimpa Yesu nguvu za kufanya miujiza. Hilo lilionekana katika kisa cha “mwanamke aliyekuwa na mtiririko wa damu kwa miaka kumi na miwili.” Ingawa “alikuwa ameumizwa sana na matabibu wengi na alikuwa ametumia mali zake zote,” kwa kweli hali yake iliendelea kuwa mbaya zaidi. Mwanamke huyo aliingia katikati ya umati na kumgusa Yesu—tendo ambalo lilivunja Sheria iliyohusu mtu mwenye ‘mtiririko wa damu.’ (Law. 15:19, 25) Yesu akatambua kwamba nguvu zilikuwa zimemtoka na hivyo akauliza ni nani aliyekuwa amemgusa. “Akiogopa na kutetemeka” mwanamke huyo “akaanguka chini mbele yake, akamwambia kweli yote.” Akitambua kwamba Yehova alikuwa amemponya mwanamke huyo, Yesu alimtendea kwa fadhili na kusema: “Binti yangu, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, na uwe na afya njema kutokana na ugonjwa wako wenye kuhuzunisha.”—Marko 5:25-27, 30, 33, 34.

  • Ni Nani Anayeweza Kuwakomboa Wale Wanaolilia Msaada?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Agosti 15
    • Anatujali kwa Huruma

      14, 15. Tunajua jinsi gani kwamba Yesu anaelewa hisia za wanadamu na kwamba “atamkomboa maskini anayelilia msaada”?

      14 Wanadamu wenye dhambi wako katika hali ya kusikitisha na wanahitaji sana msaada. Lakini tuna tumaini. (Soma Zaburi 72:12-14.) Yesu, yule Sulemani Mkuu Zaidi, anatuhurumia kwa sababu anaelewa hali yetu ya kutokamilika. Zaidi ya hayo, Yesu aliteseka kwa ajili ya uadilifu, na Mungu alimruhusu apambane na majaribu akiwa peke yake. Kwa kweli, Yesu aliteseka sana kihisia hivi kwamba “jasho lake likawa kama matone ya damu yakianguka chini”! (Luka 22:44) Baadaye akiwa kwenye mti wa mateso, alilia hivi kwa sauti: “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?” (Mt. 27:45, 46) Ingawa aliteseka sana, na hata ingawa Shetani alijitahidi kabisa kumfanya amwache Yehova, Yesu alithibitika kuwa mwaminifu kwa Yehova Mungu.

      15 Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yesu anaona uchungu tunaohisi na kwamba “atamkomboa maskini anayelilia msaada, pia mwenye kuteseka na yeyote ambaye hana msaidizi.” Akiwa mwenye upendo na mwenye kujali kama Baba yake, Yesu ‘atawasikiliza maskini’ na ‘atawaponya wenye mioyo iliyovunjika, naye atafunga sehemu zao zenye maumivu.’ (Zab. 69:33; 147:3) Yesu anaweza “kuusikitikia udhaifu wetu” kwa sababu “amejaribiwa katika mambo yote kama sisi wenyewe.” (Ebr. 4:15) Ni jambo zuri kama nini kujua kwamba Mfalme Yesu Kristo anatawala sasa mbinguni na anatazamia kwa hamu kuwaletea wanadamu wanaoteseka kitulizo!

      16. Kwa nini Sulemani aliwahurumia raia wake?

      16 Kwa kuwa Sulemani alikuwa na hekima na ufahamu, bila shaka ‘alimsikitikia mtu wa hali ya chini.’ Pia, maisha yake yalikuwa na matukio ya kusikitisha na kufadhaisha. Ndugu yake Amnoni alimlala kinguvu dada yake Tamari, na Absalomu ndugu ya Sulemani akaamuru Amnoni auawe kwa sababu ya uhalifu huo. (2 Sam. 13:1, 14, 28, 29) Absalomu alijaribu kunyakua kiti cha ufalme cha Daudi, lakini mapinduzi hayo hayakufaulu, naye akauawa na Yoabu. (2 Sam. 15:10, 14; 18:9, 14) Baadaye, Adoniya ndugu ya Sulemani alijaribu kunyakua ufalme. Ikiwa angefaulu, bila shaka Sulemani angeuawa. (1 Fal. 1:5) Tunajua kwamba Sulemani alielewa jinsi wanadamu wanavyoteseka na hilo linaonekana wazi katika maneno aliyosema katika sala wakati wa kuzinduliwa kwa hekalu la Yehova. Mfalme Sulemani alisali hivi kuhusu raia wake: “Wanajua kila mmoja wao pigo lake na maumivu yake mwenyewe . . . Nawe [Yehova] usamehe na kumpa kila mmoja kulingana na njia zake zote.”—2 Nya. 6:29, 30.

      17, 18. Ni maumivu gani ambayo watumishi fulani wa Mungu wamekabiliana nayo, na ni nini ambacho kimewasaidia?

      17 ‘Maumivu yetu wenyewe’ yanaweza kusababishwa na matukio fulani ya wakati uliopita katika maisha yetu. Mary,a Shahidi wa Yehova ambaye ana umri wa miaka 30 na kitu, anaandika hivi: “Nina kila sababu ya kuwa na furaha, lakini mara kwa mara mambo niliyofanya zamani yananiletea hisia za aibu na zenye kuchukiza. Hisia hizo zinanifanya nihuzunike sana, na kulia, ni kana kwamba mambo hayo yote yalitendeka jana. Kumbukumbu zilizotia mizizi bado zinanifanya nilemewe sana na hisia za kwamba sifai na nina hatia.”

      18 Watumishi wengi wa Mungu wanapambana na hisia kama hizo, lakini ni nini kinachoweza kuwasaidia kupata nguvu wanazohitaji ili wavumilie? Mary anasema hivi: “Sasa familia ya kiroho na marafiki wa kweli wananiletea furaha. Pia, ninajitahidi kukazia fikira ahadi za Yehova kuhusu wakati ujao, na nina hakika kwamba vilio vyangu vya kuomba msaada vitageuzwa na kuwa vigelegele vya shangwe.” (Zab. 126:5) Tunahitaji kuweka tumaini letu katika uandalizi wa Mungu wa kutoa Mwana wake, Mtawala wake aliyechaguliwa. Ilitabiriwa hivi kumhusu: “Atamsikitikia mtu wa hali ya chini na maskini, naye ataziokoa nafsi za maskini. Ataikomboa nafsi yao kutoka katika ukandamizaji na katika jeuri, nayo damu yao itakuwa na thamani machoni pake.” (Zab. 72:13, 14) Hilo linatia moyo kama nini!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki