-
“Huruma Nyororo ya Mungu Wetu”Mkaribie Yehova
-
-
1, 2. (a) Mama hutendaje mtoto wake mchanga anapolia? (b) Ni hisia gani ambayo ni yenye nguvu zaidi kuliko huruma ya mama?
MTOTO mchanga aanza kulia usiku wa manane. Mama yake anaamka mara moja. Mama halali kwa utulivu tangu alipojifungua mtoto huyo. Amejua kutofautisha vilio mbalimbali vya mtoto wake mchanga. Kwa hiyo, kwa kawaida anaweza kujua iwapo mtoto wake anahitaji kunyonya, kubebwa, au kushughulikiwa kwa njia nyingine. Mama humshughulikia mtoto wake haidhuru sababu inayomfanya alie. Hawezi kupuuza mahitaji ya mtoto wake kwa sababu anampenda sana.
2 Huruma ya mama kwa mtoto wake ni mojawapo ya hisia zenye nguvu sana ambazo wanadamu huonyesha.
-
-
“Huruma Nyororo ya Mungu Wetu”Mkaribie Yehova
-
-
Maneno kadhaa ya Kiebrania na Kigiriki yanadokeza sifa ya huruma yenye upendo. Kwa mfano, fikiria kitenzi cha Kiebrania ra·chamʹ, ambacho mara nyingi hutafsiriwa “onyesha rehema” au “hurumia.” Kichapo kimoja cha marejeo kinaeleza kwamba kitenzi ra·chamʹ “kinaonyesha huruma nyingi na yenye upendo, kama ile tunayohisi tunapowaona wapendwa wetu au wale wanaohitaji msaada wetu wakiteseka au kuumia.” Neno hilo la Kiebrania, ambalo Yehova anatumia kujihusu, linahusiana na neno linalomaanisha “tumbo la uzazi” nalo linaweza kufasiriwa kuwa “huruma ya mama.”a—Kutoka 33:19; Yeremia 33:26.
“Je, mwanamke aweza kumsahau . . . mwana wa tumbo lake? ”
4, 5. Biblia inatumiaje hisia ambazo mama huwa nazo kwa mtoto wake mchanga kutufundisha kuhusu huruma ya Yehova?
4 Biblia inatumia hisia ambazo mama huwa nazo kwa mtoto wake mchanga kutufundisha maana ya huruma ya Yehova. Twasoma hivi kwenye Isaya 49:15: “Je! mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie [ra·chamʹ] mwana wa tumbo lake? naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.” Maelezo hayo yenye kugusa moyo yanakazia jinsi Yehova alivyo na huruma nyingi kwa watu wake. Jinsi gani?
5 Ni vigumu kuwazia kwamba mama anaweza kusahau kumnyonyesha na kumtunza mtoto wake mchanga. Kwani, mtoto mchanga ni hoi; anahitaji kupendwa na kutunzwa na mama yake usiku na mchana. Ingawa hivyo, inasikitisha kupata habari kuhusu akina mama wanaowatupa watoto wao, hasa katika ‘nyakati hizi za hatari’ kwa sababu watu hawana “shauku ya kiasili.” (2 Timotheo 3:1, 3) “Lakini mimi sitakusahau wewe,” atangaza Yehova. Yehova hakosi kamwe kuwaonyesha watumishi wake huruma nyororo. Huruma hiyo ni yenye nguvu zaidi ya hisia yenye nguvu tunayoweza kuwazia, yaani, huruma ambayo kwa kawaida mama humwonyesha mtoto wake mchanga. Haishangazi kwamba mtoa-maoni mmoja alisema hivi kuhusu Isaya 49:15: “Hili ni mojawapo, au ndilo neno linalofafanua upendo wa Mungu waziwazi zaidi katika Agano la Kale.”
-